UJENZI NA UKAMILISHAJI WA MAABARA KWENYE SEKONDARI ZA JIMBO LA MUSOMA VIJIJINI 

Ujenzi wa Miundombimu kwenye Maabara ya Sekondari Nyanja ya Kata ya Bwasi

25 March 2019
Na: Fedson Masawa
Msaidizi wa Mbunge
Jimbo la Musoma Vijijini lina Kata 21, Vijiji 68 na Vitongoji 374.
Jimbo hili kwa sasa lina Shule za Sekondari za Serikali/Kata 18 na Binafsi 2. Kutokana na Ujenzi unaoendelea wa Sekondari Mpya, ifikapo Januari 2020, Jimbo linatarajia kuwa na Jumla ya Sekondari 25 (23 za Serikali/Kata na 2 za Binafsi).
UJENZI WA MAABARA KWENYE SEKONDARI JIMBONI
Sekondari za Serikali/Kata zenye Maabara 3 (Chemistry, Physics and Biology) ZINAZOTUMIKA ni: (i) Mkirira(Maabara 3), (ii) Nyakatende(2) na (iii) Bugwema (1, yenye kutumika kwa masomo yote 3)
Sekondari zote 2 za Binafsi (RC Nyegina na SDA Bwasi) zina Maabara za masomo yote 3.
SEKONDARI ZA NYANJA  NA MUGANGO ZAANZA UKALIMISHAJI WA MIUNDOMBINU YA MAABARA ZAO
SHULE ya Sekondari Nyanja iliyopo Kata ya Bwasi imeanza ujenzi wa Miundombinu ya Maabara zao 3. Sekondari ya Mugango ya Kata ya Mugango nayo iko kwenye zoezi hilo.
Maabara ya Sekondari Nyanja ina Jumla ya Vyumba vitatu ambavyo Bodi ya Shule hiyo imeamua kukamilisha Chumba kimoja ili kiwe ni cha Mfano na badae waendelea na ukamilishwaji wa Vyumba vingine viwili.
Ujenzi huu wa Miundombinu ya Maabara unafanikishwa kwa NGUVU za WANANCHI
WADAU wa MAENDELEO mbalimbali WANAOMBWA WACHANGIE UJENZI na UKAMILISHAJI WA MAABARA HIZI.
Mwezi Januari 2019, Mbunge wa Jimbo Prof Sospeter Muhongo alitembelea MAABARA za Sekondari Nyanja na Mugango na atazitembelea tena mwezi ujao, April 2019 na kuendelea kuchangia ukamilishwaji wa MAABARA hizo.
Mkuu wa Shule ya Sekondari Nyanja Mwl Charles F. Ndebele  amesema Sekondari ya Nyanja ina Jumla ya Wanafunzi 510. Wanafunzi wanaosoma Masomo ya Sayansi ni WACHACHE MNO – Form IV ni 11 na Form III ni 15.
Mwalimu Mkuu huyo  amewashukuru Wananchi, Wadau wa Maendeleo wakiwemo Diwani wa Kata yao, Mbunge wa Jimbo, Mkurugenzi wa Halmashauri na Mkuu wa Wilaya ya Musoma Dr. Vincent Naano kwa kuchangia na kusimamia Maendeleo ya Elimu Musoma Vijijini
Mbali na Maabara hiyo, Mbunge wa Musoma Vijijini Prof Muhongo amewahi kuchangia Saruji, Mabati, Madawati, Vitabu kwa Shule za Kata ya Bwasi na Mbegu za Alizeti, Mihogo na Mtama. Pampu kwa ajili ya Kilimo cha Umwagiliaji ilinunuliwa kutoka kwenye Fedha za Mfuko wa Jimbo.
Iwapo unapenda kuchangia ujenzi wa Maabara hizo, Wasiliana na:
Headmaster
Nyanja Secondary School
+255 754 404 349
+255 679 359 957