UJENZI WA SHULE SHIKIZI BUSAMBARA UMEPATA MSUKUMO MPYA BAADA YA KUSUASUA KWA MIEZI KADHAA

UJENZI wa SHULE SHIKIZI BUSAMBARA unaoendelea na utakamilika ifikapo tarehe 30 Machi 2019.

Jumamosi, 09.03.2019
Jimbo la Musoma Vijijini
Ujenzi wa Shule SIHIKIZI BUSAMBARA iliyoko Kitongoji cha Ziwa, Kijiji cha Mwiringo umepata msukumo  na mwamuko mpya baada ya kushindwa kukamilika tarehe 28 Februari 2019.
Kamati ya Ujenzi na Fundi wao, wametoa AHADI ya kukamilisha ujenzi huo ifikapo tarehe 30 Machi 2019.
Tunaomba WANANCHI waendelee KUJITOLEA kukamilisha MRADI huu wakiweka maanani kwamba SERIKALI yetu imetoa MCHANGO MKUBWA wa Tsh 60 Milioni kwenye MRADI wa  Ujenzi wa Shule SHIKIZI BUSAMBARA.
TUNAENDELEA kutoa SHUKRANI ZETU za DHATI kwa SERIKALI yetu kwa kutoa MICHANGO MIKUBWA kwa UJENZI wa SHULE SHIKIZI za Vitongoji vya Egenge, Kijiji cha Busamba (Tsh 60 M ujenzi umekamilika), Kaguru, Kijiji cha Bugwema  (Tsh 60M, ujenzi unaendelea), Mwikoko, Kijiji cha Chitare (Tsh 60M, ujenzi unakaribia kukamilika).
Vilevile tunapenda kuendelea KUPONGEZA WANANCHI walioamua KUTATUA TATIZO la UMBALI MKUBWA (Km 2 hadi 5 au zaidi) ambao WATOTO WAO wanautembea kwenda Masomoni kwenye Shule za Jirani.
WANANCHI WAMEAMUA kujenga Shule Shikizi ambazo baadae zitapanuliwa na kuwa Shule za Msingi ndani ya Vitongoji na Vijiji vyao.
Mbali ya hizo zilizotajwa hapo juu, Shule Shikizi nyingine zinajengwa:
*Kitongoji cha Kiunda, Kijiji cha Kamguruki
*Kitongoji cha Binyago, Kijiji cha Kabegi
*Kitongoji cha Gomola, Kijiji cha Musanja
*Kitongoji cha Chirugwe, Kijiji cha Buanga
*Kitongoji cha Mwaloni, Kijiji cha Buraga
JIMBO LA MUSOMA VIJIJINI LITAENDELEA KUSHIRIKIANA NA SERIKALI kwa karibu sana KUJENGA na KUBORESHA MIUNDOMBINU ya ELIMU na AFYA kwa manufaa ya Wananchi wa Vijijini mwetu na kwa WATANZANIA wote.