S/M RUKUBA YAKARIBIA KUKAMILISHA UJENZI WA MAKTABA YAO – MFANO WA KUIGWA NA SHULE NYINGINE

Maktaba ya S/M Rukuba. Inakamilishwa ujenzi

Shule ya Msingi (S/M) Rukuba iliyoko Kisiwani Rukuba ina MAENDELEO MAZURI kwenye UJENZI na UBORESHAJI wa MIUNDOMBINU YA ELIMU kama ifuatavyo:
(1) Wanafunzi wote (465, March 2019) wanasomea ndani ya Vyumba vya Madarasa. Hawapo wanaosemea CHINI ya MITI.
(2) Shule ina Vyumba 7 vya Madarasa vinavyotumika na ujenzi wa VIPYA 3 unakamilishwa. Kwa hiyo ifikapo 30 March 2019, S/M Rukuba itakuwa na Vyumba 10 vya Madarasa.
(3) Wanafunzi wote 465 wanatumia MADAWATI wakati wakiwa Madarasani. Hayupo anaekaa sakafuni.
(4) Mwalimu Mkuu anayo Ofisi yake pekee. Walimu wengine wanayo Ofisi yao. Walimu hawana Ofisi chini ya Miti.
(5) Walimu wote wanaishi kwenye NYUMBA za SHULE – Makazi ya uhakika.
(6) Shule inakamilisha ujenzi wa MAKTABA itakayotumiwa na Wanafunzi, Walimu, Wakazi na Wageni Kisiwani hapo. Itafunguliwa April 2019 wakati wa Sherehe za PASAKA za Jimbo zitakazofanyika Kisiwani hapo.
(7) Wanafunzi wanapata CHAKULA shuleni kwa siku zote za masomo.
Kisiwa cha Rukuba kina ZAHANATI inayotoa Huduma za Afya.