UFAULU MDOGO NA UMBALI MKUBWA WA SHULE ZA JIRANI VIMEWAFANYA WAKAZI WA KITONGOJI CHA MWALONI KUAMUA KUJENGA SHULE YAO

Wananchi wakiwa kazini – Urekebishaji wa Msingi na Umwagiliaji Matofali.

Jumamosi, 02.03.2019
Na: Fedson Masawa
Msaidizi wa Mbunge
Kitongoji cha Mwaloni kiko ukingoni mwa Ziwa Victoria ndani ya Kijiji cha Buraga, Kata ya Bukumi.
Wanafunzi wa Kitongoji cha Mwaloni wanasoma Shule za Msingi za jirani: S/M Buraga, mwendo km 3-4 na S/M Chitare, mwendo wa km 2-3.
Kwa Matokeo ya Mitihani ya Darasa la VII ya Mwaka jana (2018), Wanafunzi kutoka Kitongoji cha Mwaloni waliokuwa wanasoma S/M Buraga HAYUPO aliyefaulu Mitihani na kuchaguliwa kwenda Sekondari. Kwa wale waliokuwa wakisoma S/M Chitare ni WAWILI (2)  tu waliofaulu na kuchaguliwa kwenda Sekondari ya Makojo.
Kutokana na hali hiyo ya Elimu ya kutoridhisha kwenye Kitongoji cha Mwaloni, WAKAZI wa Kitongoji hicho WAMEAMUA kujenga Shule yao ya Msingi wakianzia kwa kujenga SHULE SHIKIZI ambayo itawatoa nje WANAFUNZI 34 wa Kitongoji hicho wanaosomea CHINI ya MITI.
Mwenyekiti wa Kijiji cha Buraga, Ndugu Geliad Mageta ameeleza kamba tayari ufyatuaji wa awali wa MATOFALI umekamilika baada ya kupokea SARUJI MIFUKO 50 iliyonunuliwa na Halmashauri kutoka Fedha za MFUKO wa JIMBO.
MDAU wa Maendeleoa amechangia SARUJI MIFUKO 5 iliyonunuliwa Kijijini Chitare na kukabidhia tarehe 25.02.2019 kwa Viongozi wa Kitongoji cha Mwaloni.
Ndugu Nyajoge Chirya, Mwenyekiti Kamati ya Ujenzi wa Shule hiyo, alisema kuwa SARUJI MIFUKO 5 iliyopokelewa kutoka kwa Mdau wa Maendeleo Jimboni ni MCHANGO muhimu sana kwa ujenzi wa Shule yao ambayo sasa wanaanza kunyanyua BOMA.
Mbunge wao Prof Muhongo aliahidi kuwachangia SARUJI MIFUKO 100 iwapo Halmashauri itaridhia marekebisho ya ujenzi huo
Mbali ya MICHANGO ya Mbunge Prof Sospeter Muhongo ya Madawati, Vitabu, Saruji na Mbegu za Alizeti, Mihogo na Mtama kwa  Kata ya Bukumi, Mbunge huyo wa Jimbo amechangia HUDUMA za AFYA kama ifuatavyo:
(i) SARUJI MIFUKO 50 kwenye ujenzi wa Nyumba ya Mganga wa Zahanati ya Kurugee.
(ii) Gari la Wagonjwa (AMBULANCE) la Zahanati ya Kurugee.
Vilevile Fedha za MFUKO wa JIMBO zilitumika kununua VIFAA VYA KUMWAGILIA (Kilimo cha Bustani) kwa KIKUNDI cha ANGAZA –  Pampu, Mipira na Mbegu.