JIMBO LA MUSOMA VIJIJINI – UJENZI WA ZAHANATI WAZIDI KUSHIKA KASI JIMBONI

Wananchi na Mafundi wakiendelea na Ujenzi wa Msingi wa Boma la Zahanati ya Kakisheri

Na: Fedson Masawa
Msaidizi wa Mbunge
*Tarehe 01.03.2019*
UJENZI wa Zahanati Mpya umezidi kushika kasi ndani ya Jimbo la Musoma Vijijini ili kujihakikishia upatikanaji wa Huduma bora za Matibabu (Afya) Jimboni. Hii ni sehemu muhimu ya Utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM (2015-2020).
Hali hii imedhihirika baada ya Vijiji mbalimbali kuongeza kasi zaidi na kushiriki kwa hali na mali katika ujenzi wa ZAHANATI za VIJIJI vyao.
Zahanati ya Kijiji cha Kakisheri kilichopo Kata ya Nyakatende ni moja kati ya Zahanati 13 ambazo ujenzi wake unaendelea kwa kasi kubwa. Hadi kufikia March 4, 2019 ujenzi wa Msingi wa Boma la Zahanati ya Kakisheri utakuwa umekamilika.
Zahanati nyingine zinazoendelea kujengwa Jimboni ni (ii) Zahanati ya Kijiji cha Bukumi inayojengwa kwenye Kitongoji cha Burungu. Vijiji vingine vinavyojenga Zahanati zao ni: (iii) Butata, (iv) Chimati, (v) Chirorwe, (vi) Kurwaki, (vii) Maneke, (viii) Mkirira, (ix) Mmahare, (x) Nyasaungu, (xi) Muhoji, (xii) Kurukerege na (xiii) Bwai Kwitururu.
Akizungumza na Msaidizi wa Mbunge, kwa niaba ya Wana-Kakisheri,  kwenye eneo la ujenzi huo, Mwenyekiti wa Serikali ya Kijiji Ndugu Msafiri Corrence amesema, Wananchi wa Kakisheri WAMEAMUA KWA DHATI kuchangia ujenzi wa Zahanati yao ili ikamilike na kuanza kutoa huduma ifikapo January 2020.
Mwenyekiti pia ameshukuru jitihada za Mbunge Prof Muhongo za kuchangia shughuli za Maendeleo Kijijini Kakisheri, MICHANGO hiyo ni pamoja na:
(i) Madawati 99 kwa S/M Kambarage
(ii) Mabati 54 kwa S/M Kambarage
(iii) Saruji Mifuko 60 kwa S/M Kambarage
(iv) Vitabu vingi
(v) Mbegu za Mihogo, Mtama na Alizeti.
Pamoja na Michango hiyo, Wananchi wamezidi kuwaomba Ndugu na Jamaa, Wadau mbalimbali wa Maendeleo ndani na nje ya Jimbo washirikiane na WAKAZI wa Kijiji cha Kakisheri, Kata ya Nyakatende kuchangia ujenzi wa ZAHANATI ya Kijiji hicho ili kufikia malengo yao ya kuanza kuitumia ifikapo Januari mwakani (2020)