WANANCHI WA KIJIJI CHA WANYERE WAENDELEA NA UJENZI WA VYUMBA VIPYA VYA MADARASA

Wananchi wa Vitongoji vya Mwikoro na Komesi wakiendelea na ujenzi wa Msingi wa Vyumba Vipya 2 vya Madarasa ya Shule ya Msingi ya Wanyere A.

Na: Hamisa Gamba
Msaidizi wa Mbunge
Kata ya Suguti inaundwa na Vijiji vinne (4), ambavyo ni Kusenyi, Suguti, Chirorwe na Wanyere.
Kijiji cha Wanyere kina VITONGOJI SITA (6) na Shule za Msingi (S/M) tatu (3) – S/M Wanyere A, S/M Wanyere B, na S/M Murugee.
Kijiji cha Wanyere kimeanza ujenzi wa Vyumba Vipya vya MADARASA kwa Shule zake za  Msingi kwa  MPANGILIO na MGAWANYO ufuatao:
(i) S/M Wanyere A: Vitongoji vya Mihuru na Mururangu – Wananchi wa Vitongoji hivi wanaendelea na ujenzi wa Msingi wa Vyumba vya Madarasa, na wanataraji kukamilisha ujenzi huu ifikapo Alhamisi, 21.02.2019 (kesho)
(ii) S/M Wanyere B: Vitongoji vya Mwikoro na Komesi – Wananchi wa Vitongoji hivi tayari WANAPAUA Vyumba vya Madarasa.
(iii) S/M Mrugee: Vitongoji vya Ambagai na Mrugee yenyewe – Wananchi  wameanza uchimbaji wa Msingi, na matarajio yao ni kuanza ujenzi wa Msingi kabla ya Ijumaa ya wiki hii (kesho kutwa)
Mwenyekiti wa Kijiji cha Wanyere, Ndugu Charles Mtani alieleza kuwa wameamua kuendesha UJENZI huo kwa kugawanya kazi kwa VITONGOJI na hivyo kufanya USHINDANI kati ya Vitongoji ili KUHARAKISHA ujenzi wa Vyumba Vipya vya Madarasa. Lengo ni kuhakikisha kila Kitongoji HAKINA Shule ambayo WANAFUNZI wanasomea nje CHINI ya MITI kwa kukosa Vyumba vya MADARASA.
Mbunge wa Jimbo Prof Sospeter Muhongo ameishatoa MICHANGO kadhaa kwa Shule zote 3 kama ifuatavyo: (a) Jumla ya Madawati 293, (b) Jumla ya Vitabu Box 30 (zaidi ya vitabu 1,500), (c) Jumla ya SARUJI MIFUKO 145. Mfuko wa Jimbo umechangia Jumla ya SARUJI MIFUKO 100 na Mabati 58 (S/M Wanyere B).
Diwani wa Kata hiyo ya Suguti, Mhe Dennis Ekwabi ameendelea kusisitiza WANANCHI wa Kata hiyo kuendelea kufanya kazi kwa kushirikiana, kwa kujituma na bila Malumbano. Hii itasaidia kuyatimiza yale waliyojipangia. Aidha pia Mheshimiwa huyo, anaendelea kutoa shukrani za pekee kwa Mbunge wa Jimbo la Musoma Vijijini, Mhe. Prof Muhongo kwa MIRADI anayoendelea kuitekeleza Jimboni, na pia kwa WANANCHI kwa KUJITOLEA kwao. Ameshukuru Mfuko wa Jimbo akiamini kuwa hizi ni jitihada za SERIKALI  kuunga mkono juhudi za Wananchi za kujitolea kujiletea MAENDELEO yao wenyewe.