MBUNGE ACHANGIA SARUJI KATIKA UJENZI WA VYUMBA VYA MADARASA YA S/M RWANGA.

Majengo yanayojengwa kwa MICHANGO ya Wananchi, Mbunge wa Jimbo na Mradi wa EQUIP. Majengo haya yatakamilika tarehe 28.02.2019.

Jumapili 24. 2.2019
Na: Hamisa Gamba
Msaidizi wa Mbunge
Kijiji cha Kasoma ni kati ya Vijiji 5 vinavyounda Kata ya Nyamrandirira. Vijiji vingine ni Mikuyu, Seka, Chumwi na Kaboni
Leo Jumapili, tarehe 24.02.2019 Mbunge wa Jimbo Prof Sospeter Muhongo amekabidhi SARUJI MIFUKO 50, akiwa anatimiza AHADI YAKE aliyoitoa hivi karibuni wakati alipotembelea S/M Rwanga.
Afisa Mtendaji wa Kijiji hicho Ndugu Faustin M. Majura amesema kuwa S/M RWANGA ni shule changa iliyoanzishwa Mwaka 2016, na hadi sasa ina jumla ya Wanafunzi 319 wa Darasa la I – IV. Ina  jumla ya Vyumba vya Madarasa viwili (2) kwa matumizi ya Madarasa 4, kwa hiyo Wanafunzi wanasoma kwa zamu kwa kuachana madasara hayo mawili.
Afisa Mtendaji huyo aliendelea kueleza kuwa Wananchi wa Kijiji cha Kasoma WAMEAMUA KUJITOLEA kujenga Vyumba vya kutosha  ili KUTATUA TATIZO hilo.
Wananchi wanaendelea kuchanga fedha, na kusomba mawe, kokoto, mchanga na maji kwa ajili ya ujenzi huu.
Mbunge wa Jimbo Prof Muhongo aliwachangia SARUJI MIFUKO 60 iliyowasaidia kujenga Vyumba 2 vya Madarasa ambavyo vinakamilishwa. Mradi wa EQUIP (Mradi wa Ushirika wa Serikali yetu na DfID, UK) nao umechangia ujenzi wa Vyumba 2 vipya hapo shuleni.
Mwenyekiti wa Kijiji hicho, Ndugu Fedson B. Msalama ametoa shukrani za pekee kwa Mbunge wa Jimbo la Musoma Vijijini kwa moyo wake wa KUJITOLEA kuchangia  Maendeleo ya JIMBO ZIMA ikiwemo S/M Rwanga. Kiongozi huyo alibainisha MICHANGO ya Mbunge wao kwa Shule yao kwamba ni:
(i) Box 10 za Vitabu. Takribani Vtabu 500
(ii) Saruji Mifuko 60
(iii) Madawati 64
Mfuko wa Jimbo umechangia:
(iv) Mabati 54
(v) Mabati 150  yaliyogawiwa tarehe 20/2/2019 baada ya KIKAO cha WAZI cha kugawa FEDHA hizo kilichofanyika Kijijini Bugoji, Kata ya Bugoji.
SARUJI MIFUKO 50 zilizokabidhiwa leo tarehe 24/2/2019 kwa Viongozi wa Kijiji hicho, zitatumika kwenye UJENZI MPYA wa Vyumba vingine  viwili (2) vya Madarasa. Viongozi wa Kijiji wamesema kwamba ifikapo Jumatano ya tarehe 27.2.2019 Msingi (foundation) utakuwa umekamilika.
OMBI: Uongozi wa Kijiji cha Kasoma na wa S/M Kasoma wanaomba WADAU wa MAENDELEO waungane nao kuijenga S/M Kasoma.