WANANCHI WA KIJIJI CHA BUSUNGU WAAMUA KUTOKOMEZA UPUNGUFU WA VYUMBA VYA MADARASA KWENYE SHULE YAO YA MSINGI

Maendeleo ya Ujenzi wa Vyumba vya Madarasa vya Shule ya Msingi Busungu

Na: Verediana Mgoma
Msadizi wa Mbunge
Upungufu wa Vyumba vya Madarasa MASHULENI ni tatizo ambalo WANANCHI wa Jimbo la Musoma Vijijini WAMEAMUA KULITATUA kwa kushirikiana na SERIKALI yao.
Wananchi wa Kijiji cha Busungu, Kata ya Bulinga wameamua na kuanza Ujenzi wa Vyumba VIPYA vya Madarasa kuondoa uhaba wa Vyumba vya Madarasa uliopo kwenye Shule ya Msingi Busungu.
Mtendaji wa Kijiji cha Busungu, Ndugu Charles Ndagile amesema kwamba Wananchi wamehamasika kuchangia NGUVUKAZI zao ili kuondoa MIRUNDIKANO ya Wanafunzi madarasani.
 “Tumefanikiwa kunyanyua Maboma ya Vyumba 3 na Ofisi ya Walimu, tukiwa na LENGO la kuondoa kabisa tatizo la UKOSEFU wa Vyumba vya Madarasa kwenye Shule yetu,” alisema Ndugu Charles Ndagile.
Kwa upande wake, Mwalimu Mkuu wa Shule hiyo, Ndugu Chacha Magogo alitoa taarifa ya Shule yake na kusema kwamba Shule ina Jumla ya  Wanafunzi 570, ina Madarasa 7 na ina upungufu wa Madarasa 5. S/M Busungu inamshukuru sana Mbunge Prof Muhongo kwa kuchangia SARUJI MIFUKO 110.
“Hatuna Wanafunzi wanaosomea nje chini ya MITI,  lengo letu ni KUONDOA MIRUNDIKANO ya Wanafunzi Madarasani ili kila Darasa lichukue Wanafunzi 45, ” alisema Mwalimu Mkuu, Ndugu Charles Magogo.
Aidha Diwani wa Kata ya Busungu, Ndugu Mambo Japani ameishukuru SERIKALI kwa MISAADA iliyotoa kwenye ujenzi wa Shule za Msingi na Sekondari kwenye Kata hiyo. Vilevile amemshukuru  Mbunge wa Jimbo Prof Sospeter Muhongo kwa MICHANGO aliyotoa kwenye Kata hiyo ikiwemo ya MADAWATI, VITABU na MBEGU za MAZAO (Alizeti, Mihogo na Mtama),.
Diwani wa Kata Mhe Mambo Japani anasisitiza na kusema kwamba WAMEAMUA kuboresha MIUNDOMBINU YA ELIMU kwenye Shule zote za Msingi zilizoko ndani ya Kata yao. Aliendelea kutoa SHUKRANI NYINGI kwa Halmashauri na SERIKALI kwa ujumla kwa kuungana na  Wananchi, yeye mwenyewe (Diwani) na Mbunge wa Jimbo kukamilisha ujenzi wa Sekondari Mpya iliyoanza kuchukua Wanafunzi wa Form I Mwaka huu (Jan 2019). Wanakamilisha usajili wa Sekondari hiyo ya Kata (Bulinga Secondary School).