UJENZI NA UBORESHAJI WA MIUNDOMBINU YA ELIMU JIMBONI MWETU NI WA LAZIMA KUFANYIKA SASA NA KWA KASI KUBWA

Vikao vya Wanavijiji wa Kata ya Suguti (Vijiji 4) na Mbunge wao Prof Sospeter Muhongo

Mh. Mbunge Prof Sospeter Muhongo alikuwa kwenye Kata ya Suguti yenye Vijiji 4 (Wanyere, Chirorwe, Kusenyi na Suguti).
Hali ya Miundombinu ya Elimu kwenye Kata ya Suguti, yenye Vijiji 4 na Sekondari 1 ya Kata, inafanana na hali iliyoko kwenye Kata nyingine 18 alizozitembelea Mbunge wa Jimbo.
MIFANO YA KUHUZUNISHA:
(1) S/M Wanyere A iliyoanza kutoa elimu Mwaka 1954, yenye Wanafunzi 537 ina Vyumba vya Madarasa 5 na pungufu 7. Watahiniwa (2018) walikuwa 48, Waliofaulu na kuchaguliwa kwenda Form I ni 18.
(2) S/M Murugee (1996), Wanafunzi 350, Madarasa 6 na pungufu 4. Watahiniwa 36, Waliofaulu na kuchaguliwa 14.
(3) S/M Suguti A (1946), Wanafunzi 638, Madarasa 7 na  pungufu 5. Watahiniwa 62, Waliofaulu 30, Waliochaguliwa 11.
UAMUZI WA WANANCHI NA VIONGOZI WAO
(1) Ujenzi wa Vyumba Vipya vya Madarasa HAUKWEPIKI, NI WA LAZIMA!
(2) Maboma yanayojengwa YAKAMILISHWE KABLA ya Tarehe 30 January 2019. Ujenzi mpya utakaoanza wiki ijayo ukamilike ifikapo 28 February 2019… Marshall Plan of its kind?
HARAMBEE na MICHANGO YA MBUNGE
Utaratibu wa Mbunge wa Jimbo Prof Muhongo ni kwamba ANACHANGIA pale ambapo ujenzi UMEANZA na una RATIBA YA UJENZI inayotekelezeka.
Kwa leo, Jumanne, tarehe 08.01.2019, Mbunge wa Jimbo amechangia (kutegemeana na Ratiba zao za ujenzi zilizokubalika mbele ya Vikao na Mbunge wao):
(1) S/M Murugee
Saruji Mifuko 50
(2) S/M Wanyere B
Mabati 54
(3) S/M Wanyere A&B:
Saruji Mifuko 50
(4) S/M Kusenyi A
Mabati 54
(5) S/M Kusenyi B
Saruji Mifuko 20
(6) S/M Suguti A
Saruji Mifuko 50
(7) S/M Suguti B
Saruji Mifuko 50