WANAFUNZI 232 NDANI YA CHUMBA KIMOJA CHA DARASA – WANANACHI WAAMUA KUTATUA MATATIZO YA UKOSEFU WA VYUMBA VYA MADARASA MASHULEN

Kikao cha Wanakijiji na Mbunge wao Prof Muhongo wakiwa kwenye eneo la ujenzi wa SHULE MPYA YA MSINGI kwenye Kitongoji cha Gomora, Kijiji cha Musanja, Kata ya Musanja.

Jumatatu, 07.01.2019, Mbunge Prof Sospeter Muhongo AMEENDELEA na Ziara zake za KUKAGUA na KUPIGA HARAMBEE  za Ujenzi na Uboreshaji wa Miundombinu ya ELIMU na AFYA Jimboni. Leo alikuwa kwenye Kata za Musanja na Murangi.
Matatizo ya Miundombinu ya Elimu yanafanana sana kwa karibu Kata zote 21, na Vijiji vyake 68.
MIFANO INAYOTULAZIMISHA SISI SOTE KUBADILIKA NI HII:
(1) UPUNGUFU WA VYUMBA VYA MADARASA – (a) S/M Nyabaengere (ilianzishwa Mwaka 1996), pungufu vyumba 13,  (b) S/M Kanyega (1952), pungufu vyumba 11
(2) WANAFUNZI (STD VII, 2018) WALIOFAULU vs WALIOCHAGULIWA –
 (a) S/M Murangi B Waliofaulu 21
Waliochaguliwa 5
(b) S/M Lyasembe
Waliofaulu 33
Waliochaguliwa 9
(c) S/M Kanyega
Waliofaulu 61
Waliochaguliwa 30
MFANO WA MATOKEO KIDATO CHA IV (2017)
Mabui Merafuru Secondary School (35 in 2017)
(a) Division III: 3
(b) Division IV: 16
(c) Division 0: 16
Nyumba za Walimu – pungufu 15
Padre anakusudia KUFUNGA HOSTEL ya Wasichana wa Mabui Secondary kwa sababu WAZAZI HAWATAKI WATOTO WAO WAKAE HOSTEL WAKATI WA MASOMO – sababu kuu ni: hawataki kuchangia gunia moja la mahindi kwa mwaka mmoja wa masomo  n.k.
WANANCHI/WAZAZI WAMEKUBALI KUBADILIKA KAMA IFUATAVYO:
(1) Kujenga Vyumba vya Madarasa kwa kasi kubwa na kukamilisha ujenzi huo ifikapo tarehe 30 Jan 2019.
(2) Wanafunzi wote waliofaulu kuendelea na masomo ya Sekondari, wajiunge na Sekondari za Kata zao ifikapo 01.02.2019
(3) Ujenzi wa Vyumba VIPYA vya Madarasa kwenye Shule za Msingi na Sekondari UTAKUWA ENDELEVU KWA MIAKA KADHAA
(4) Msongamano ukiwa mkubwa SHULE MPYA ZIJENGWE, k.m. Mbunge ataweka (28.02.2019) Jiwe la Msingi  la Shule MPYA ya Msingi Kijijini Musanja.
HARAMBEE, MICHANGO & AHADI ZA MBUNGE ZA TAREHE 07.01.2019
(1) Vijiji ambavyo havijaanza ujenzi vianze haraka na Mbunge Prof Muhongo ATAPIGA HARAMBEE za ujenzi  wao.
(2) S/M Nyabaengere, Kata ya Musanja. (a) Saruji Mifuko 60, (b) Mabati 108 (wakiwa tayari kuezeka)
(3) S/M (Mpya) Sombero, Kata ya Musanja. Saruji Mifuko 100 (awamu 2)
(4) Murangi Sekondari. Saruji Mifuko 100 (awamu 2).  Vyumba  Vipya vya Madarasa 2 vikalike na kuanza kutumika ifikapo tarehe 01.02.2019.