WANAFUNZI WA DARASA LA 7 JIMBONI WANAFAULU LAKINI WANACHAGULIWA WACHACHE KUENDELEA NA MASOMO YA SEKONDARI KUTOKANA NA UPUNGUFU MKUBWA WA VYUMBA VYA MADARASA KWENYE SEKONDARI ZA KATA

Baadhi ya Matukio ya ziara ya tarehe 06.01.2019 ya Mbunge Prof Muhongo Kata za Bwasi na Bukima

Kwenye Vikao kati ya Wanavijiji/Wazazi na Mbunge wao Prof Sospeter Muhongo, TATIZO LA UKOSEFU/UPUNGUFU wa Vyumba vya Madarasa kwenye Sekondari za Kata LIMEPATIWA SULUHISHO – UJENZI WA VYUMBA VIPYA.
Ziara ya  Jumapili (06.01.2019) kwenye Kata za Bwasi na Bukima IMEWEKA MSUKUMO MKUBWA WA KUHAKIKISHA Wanafunzi Waliofaulu Mitihani ya Darasa la VII Mwaka Jana (2018), WANACHAGULIWA WOTE KUENDELEA NA MASOMO YA SEKONDARI IFIKAPO tarehe 30 Januari 2019.
Mfano: S/M Bukima A – Waliofaulu ni 41, Waliochaguliwa ni 11 (26.8% ya Waliofaulu). Wanafunzi 30 (73.2% ya Waliofaulu) wamebaki nyumbani wakisubiri nafasi kupatikana kwenye Sekondari ya Bukima ni 30!
UTATUAJI WA TATIZO LA UPUNGUFU/UKOSEFU WA VYUMBA VYA MADARASA KWENYE SEKONDARI ZA KATA –
(1) Jumla ya Sekondari za /Kata/Serikali (Jan 2019) ni: 19 ikiwemo Sekondari Mpya ya Bulinga –  Kila Sekondari ya Kata inajenga Vyumba vya Madarasa 2 (au zaidi) ambavyo vinatarajiwa kukamilika tarehe 15 Jan 2019 au tarehe 30 Jan 2019. Sekondari ya Bukima inaweza kukamilisha Vyumba 3.
(2) Sekondari Mpya zinajengwa kwa kasi kubwa ili zianze kutumika Mwaka huu (2019), ambazo ni 2: Sekondari za Busambara (Kata ya Busambara na Bugoji (Kata ya Bugoji, imependekezwa iitwe, “Dan Mapigano Memorial Secondary School”)
UPUNGUFU/UKOSEFU WA VYUMBA VYA MADARASA KWENYE SHULE ZA MSINGI  –
Tatizo la Wanafunzi kusomea CHINI ya MITI (zaidi ya 13,000) na Msongamano Madarasani (50-200) wa Wanafunzi wa Shule za Msingi nalo LINATATULIWA KWA KUJENGA VYUMBA VIPYA vya Madarasa kwenye Shule za Msingi za Jimboni (112, ikiwemo 1 ya Binafsi)
Mfano: Kijiji cha Bugunda – S/M Bulinga A&B: Wanafunzi wanaosomea CHINI YA MITI ni 615!
Hata S/M Bwasi iliyoanzishwa Mwaka 1952 bado inapungufu mkubwa wa Vyumba vya Madarasa!
MICHANGO YA UJENZI WA VYUMBA VIPYA VYA MADARASA KWENYE SHULE ZA MSINGI na SEKONDARI
Wanavijiji kwenye Vijiji vingi (jumla 68) WAMEAMUA KUJITOLEA kwenye ujenzi huu. Vipo vijiji vichache sana ambavyo MWITIKIO ni HAFIFU!
Wanavijiji wa Kata za Bwasi na Bukima wameendelea kuchangia fedha na kusomba mawe, kokoto, mchanga na maji kwenye ujenzi huu.
Mbunge Prof Muhongo ameendelea na HARAMBEE kwa ajili ya ujenzi huu na tarehe (06.01.2019) alichangia kama ifuatavyo:
(i) S/M Bwasi – wanavijiji hawajahamasika kutoa michango. Wanajipanga na watamwita Mbunge apige Harambee.
(ii) S/M Kome, Kata ya Bwasi: Mabati 72
(iii) Nyanja Sec School, Kata ya Bwasi: vifaa vya ujenzi vya Maabara – ujenzi ukianza na kuvibainisha.
(iv) Bukima Sec School, Kata ya Bukima: Saruji Mifuko 50.
(v) S/M Mkapa, Kijiji cha Kastamu, Kata ya Bukima: Saruji Mifuko 100 (awamu 2) wakianza ujenzi wiki ijayo.