WANANCHI WA JIMBO LA MUSOMA VIJIJINI WAMEAMUA KUSHIRIKIANA NA SERIKALI KUBORESHA MIUNDOMBINU YA ELIMU JIMBONI MWAO

Mbunge Prof Muhongo akizungumza na WANAVIJIJI wa Kata za Nyamurandirira na Nyakatende

UKAGUZI na HARAMBEE za Ujenzi  na Uboreshaji wa MIUNDOMBINU ya ELIMU Jimboni – Mbunge wa Jimbo Prof Sospeter Muhongo AMEENDELEA KUSISITIZA UMUHIMU wa Upatikanaji wa kutosha na unaokubalika wa Vyumba vya Madarasa kwenye Shule za Msingi na Sekondari.
Msisitizo huo aliendelea kuutoa wakati wa ziara zake  kwenye Kata za Nyamurandirira na Nyakatende.
Kuna TOFAUTI KUBWA SANA za MWITIKIO na USHIRIKI wa Kata na Vijiji vyake kwenye masuala ya MAENDELEO. Mifano ni hiyo hapo chini:
(1) Vyumba vya Madarasa kwenye Shule za Msingi vina wanafunzi kati ya 50 na 150 au zaidi kwenye chumba kimoja. Hii ni hali halisi kwenye kila Kata (tunazo Kata 21, Vijiji 68).
(2) Bado wapo Wanafunzi (zaidi ya 13,000) ndani ya Jimbo letu wanaosemea chini ya miti.
(3) Shule nyingi za Msingi zina upungufu mkubwa wa Vyumba vya Madarasa, kwa hiyo kuna Madarasa yanasoma kwa zamu (shift), asubuhi/mchana.
(4) Kata ya Nyamurandirira yenye Vijiji 5 (Mikuyu, Seka, Chumwi, Kasoma na Rwanga) inayo Sekondari 1 (Kasoma) ambayo ni ya Serikali. Sekondari ya Kasoma yenye Kidato cha I hadi VI ilianza kama Middle School Mwaka 1956. Kwa hiyo Vijiji vyote 5 vya Kata ya Nyamurandirira vinategemea Sekondari moja ya Serikali.
Matokeo yake, kwa Mwaka huu (Jan 2019):
(a) S/M Mikuyu: Wanafunzi 1 tu amechaguliwa kwenda Form I Kasoma Sekondari.
(b) S/M Nyamurandirira: wanafunzi 3 tu ndio wamechaguliwa kwenda Kasoma Sekondari
(c) S/M Chumwi A:
Wanafunzi 19 kati ya 33 Waliofaulu ndio wamechaguliwa kwenda Kasoma Sekondari.
SULUHISHO:
Mbunge Prof Muhongo ameshauri: (a) Vijiji vya Seka, Chumwi na Rwanga VIJENGE Sekondari zao KUPUNGUZA msongamano kwenye Sekondari ya Kasoma.
(b) Wananchi waendelee kujenga kwa kasi kubwa  Vyumba Vipya vya Madarasa kwenye Shule za Msingi na Sekondari.
(c) Mbunge wa Jimbo Prof Muhongo AMEPIGA HARAMBEE ya Ujenzi wa Vyumba Vipya vya Madarasa kwenye Maboma yanayokusudiwa kukamilika kabla ya tarehe 30 Januari 2019.
(d) HARAMBEE na MICHANGO YA UJENZI
Wanavijiji wanaendelea kusomba mawe, kokoto, mchanga na maji. Vilele wanachangia fedha za ununuzi wa vifaa vya ujenzi.
Mbunge wa Jimbo Prof Muhongo ameendelea kupiga HARAMBEE na yeye mwenyewe kuchangia kama ifuatavyo:
(i) S/M Mikuyu, Kata ya Nyamurandirira Mabati 87
(ii) S/M Rwanga, Kata ya Nyamundarira, Saruji Mifuko 100
(iii) S/M Kigera, Kata ya Nyakatende, Mabati 90
(iv) Zahanati ya Kijiji cha Kakisheri, Kata ya Nyakatende, Saruji Mifuko 100
Vifaa hivyo vya ujenzi kutoka kwa Mbunge VITANUNULIWA SIKU ambayo Wanavijiji watakuwa wako tayari (vifaa vingine vikiwepo) kukamilisha ujenzi wao kwa hatua iliyopangwa.