MBUNGE WA MUSOMA VIJIJINI AENDELEA KUSHIRIKIANA NA WANAVIJIJI JIMBONI KUJENGA NA KUBORESHA MIUNDOMBINU YA ELIMU

Prof Sospeter Muhongo AMETIMIZA AHADI YAKE YA KUCHANGIA MABATI BANDO 8, yaani Mabati 112 ya kuezekea Vyumba vya Madarasa 2 katika SEKONDARI MPYA YA KATA YA BUSAMBARA

Matokeo ya Mitihani ya Shule za Msingi na Sekondari kwenye Jimbo la Musoma Vijijini HAYARIDHISHI KABISA – ni tatizo la miaka takribani 10 iliyopita.
Matatizo ya ufaulu mbaya yanajulikana. Moja kati ya hayo ni MAZINGIRA YA KUFUNDISHIA NA KUJIFUNZIA YASIYOKUWA MAZURI kwa Walimu na Wanafunzi, hasa UKOSEFU au UPUNGUFU wa VYUMBA vya MADARASA.
Mbunge wa Jimbo Prof Sospeter Muhongo ANAENDELEA KUSHIRIKIANA na WANAVIJIJI kutatua tatizo la upungufu/ukosefu wa Vyumba vya Madarasa kwenye Shule za Msingi (112, moja ikiwa ya Binafsi) na Sekondari 20 (2 zikiwa za Binafsi).
Januari 2019, Sekondari Mpya ya Bulinga itafunguliwa.
Kata ya Busambara yenye Vijiji 3 (Mwiringo, Kwikuba na Maneke), WIKI IJAYO, ITAANZA KUEZEKA VYUMBA VYA MADARASA 4 ya SEKONDARI MPYA YA KATA HIYO. Kusudio muhimu ni Sekondari hiyo kuanza Masomo ya Form I ifikapo tarehe 01 Februari 2019. Hii itakuwa Sekondari ya 21 ndani ya Jimbo la Musoma Vijijini (19 za Serikali/Kata na 2 Binafsi).
Mtendaji wa Kata ya Busambara, Bi Sabine Peter Chacha amesema kwamba WANAFUNZI 98 wa Kata ya Busambara WAMEFAULU KUENDELEA na Masomo ya Sekondari lakini WATABAKI NYUMBANI hadi hapo nafasi kwenye Vyumba vya Madarasa itakapopatikana kwenye Sekondari za jirani (zimejaa) au kwenye hiyo ya Kata inayojengwa Kijijini Kwikuba.
Ndugu Kubega, Mwenyekiti wa Kijiji cha Kwikuba amesema kwamba dhamira ya Wanavijiji wa Kata ya Busambara ni kujenga na kukamilisha baadhi ya majengo muhimu ya awali ili watoto wao 98 waanze Form I ifikapo tarehe 01 Februari 2019.
Leo, Ijumaa tarehe 04.01.2019, Mbunge wa Jimbo Prof Sospeter Muhongo AMETIMIZA AHADI YAKE YA KUCHANGIA MABATI BANDO 8, yaani Mabati 112 ya kuezekea Vyumba vya Madarasa 2.
Wanavijiji nao wamenununua Mabati Bando 8 kuezekea Vyumba vya Madarasa 2. Kwa hiyo ndani ya Wiki 2 zijazo, Vyumba vya Madarasa 4 vya Sekondari ya Busambara vitakuwa vimeezekwa.
Wanavijiji wa Kata ya Busambara WANAENDELEA KUOMBA WADAU WA MAENDELEO wachangie angalau Mabati 54 ya kuezeka Ofisi 1ya Walimu. Wao wanaendelea kuchangia ujenzi wa Sekondari yao ya Kata.