KATA YA BUKIMA WAAMUA KUTATUA TATIZO LA UKOSEFU WA VYUMBA VYA MADARASA KWA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA MASOMO YA KIDATO CHA KWANZA

Maendeleo ya ujenzi wa Vyumba vya Madarasa vya Sekondari ya Bukima

Na: Verediana Mgoma
Msaidizi wa Mbunge
Wananchi wa Vijiji Vitatu vya Kata ya Bukima – Butata,  Kastam na Bukima VIMEAMUA KWA KAULI MOJA na wamedhamilia kukamilisha ujenzi wa Vyumba vya Madarasa ya Kidato cha Kwanza, baada ya Wanafunzi waliofaulu kujiunga na Kidato cha Kwanza kwa Mwaka huu (2019) kukosa mahali pakusomea.
Akizungumzia tatizo hilo, Mkuu wa Shule ya Sekondari  Bukima, Mwalimu  Elberth Deogratias anaeleza kwamba jumla ya Wanafunzi WALIOCHAGULIWA  kujiunga na Kidato cha Kwanza ni 187,  WALIOANZA masomo ni 50, na WANAOSUBIRI uwepo wa Vyumba vya Madarasa (vikamilike kujengwa) ni WANAFUNZI 137
Nao Viongozi wa ngazi mbalimbali wa Kata ya Bukima na Vijiji vyake 3, wamesema kuwa  WANALAZAMIKA kujenga Vyumba Viwili  vya Madarasa  na Kukarabati chumba kimoja kwa lengo la kuepusha WATOTO wao KUKAA MTAANI kwa kukosa mahali pa kusomea!
Naye Mhe January Simula ambaye ni Diwani wa Kata ya Bukima amesema  MIPANGO iliyopo ni kuhakikisha kwamba ifikapo tarehe 01.02.2019, Wanafunzi WANAOSUBIRI Vyumba vya Madarasa kupatikana Bukima Sekondari, WANAANZA MASOMO YAO ya Form I.
 Mhe Diwani Simula amesema, “Tunawashukuru WANANCHI walioamua kujitolea kwenye ujenzi huu na Mbunge wa Jimbo Profesa Muhongo aliyechangia SARUJI MIFUKO 50 kuhakikisha uhaba wa Vyumba vya Madarasa unatatuliwa kwa manufaa ya watoto wetu.”
Aidha ujenzi wa VYUMBA VYA MADARASA ni MPANGOKAZI ENDELEVU  kwa Vijiji hivyo Vitatu kwa kusudio la kuondoa UKOSEFU wa upungufu wa Vyumba vya Madarasa kwenye Shule zote (Sekondari & Msingi) ndani ya Kata hiyo.