MIUNDOMBINU YA ELIMU – UPUNGUFU WA VYUMBA VYA MADARASA NDANI YA JIMBO LA MUSOMA VIJIJINI

Wananchi na Viongozi waliohudhuria HARAMBEE ya KUPAUA Maboma 3 ya Sekondari ya Busambara

TUJIKUMBUSHE:
(a) Jumla ya Shule za Sekondari (Jan 2019): 20 (18 Serikali, 2 Binafsi)
* Chumba kimoja cha Darasa KINAPASWA kutumiwa na Wanafunzi 40
(b) Jumla ya Shule za Msingi (Jan 2019): 112 (111 Serikali, 1 Binafsi)
*Chumba kimoja cha Darasa KINAPASWA kutumiwa na Wanafunzi 45.
MATOKEO YA MITIHANI YA STD VII MWAKA HUU (2018)
(a) Wanafunzi Waliofaulu: 3,117
(b) Wanafunzi Waliochaguliwa: 1,649 (52.90%)
(c) Wanafunzi Waliokosa Nafasi: 1,468 (47.10%)
USHAURI/OMBI
(a) TUKIJENGA VYUMBA VINGI ZAIDI kwenye Sekondari zetu, Wanafunzi Waliokosa Nafasi (1,468) WATAPATA NAFASI ZA KUJIUNGA na Form I mwakani (Jan 2019)
(b)Wanafunzi wa Shule za Msingi 13,570 WANASOMEA CHINI YA MITI
WANANCHI WAMEAMUA TUTATUA TATIZO SUGU LA UKOSEFU/UPUNGUFU WA VYUMBA VYA MADARASA
(a) Wanavijiji WAMEKUBALI KUCHANGA Shilingi 15,000 kutoka kila KAYA.
(b) Wanavijiji WAMEKUBALI KUCHANGIA NGUVU ZAO kwa kusomba mawe, kokoto, mchanga na maji ya ujenzi.
Jumamosi, tarehe 15.12.2018 Mbunge wa Jimbo Prof Sospeter Muhongo AMETEMBELEA na KUKAGUA UJENZI WA VYUMBA VYA MADARASA VYA KATA 2 za KIRIBA na BUSAMBARA kama alivyofanya jana (14.12.2018 kwenye Kata za Makojo na Bulinga).
* Sekondari Mpya ya Bulinga itafungiliwa Januari 2019.
HARAMBEE (15.12.2018)
Lengo ni kupiga Harambee ili Shule ya Sekondari Busambara ikamilike na kufunguliwa January 2019.
Wananchi wamejenga na KUKAMILISHA VYUMBA vya MADARASA SITA (6) na OFISI YA WALIMU MOJA (1).
HARAMBEE ya Leo, 15.12.2018 IMEFANIKISHA kupatikana MABATI YA KUEZEKA BOMA MOJA lenye Vyumba vya Madarasa 2.
(a) Mabati ya kuezeka BOMA 1: 216
(b) Bei ya BATI 1: Shilingi 27,000
(c) Michango ya Wananchi (Harambee): Mabati 135
(d) Mchango wa Mbunge wa Jimbo (Harambee): Mabati 96 (bundle 8)