UBORESHAJI WA KILIMO CHA ZAO LA MIHOGO NDANI YA JIMBO LA MUSOMA VIJIJINI

KIKAO CHA WATAALAMU WA KILIMO NA WAKULIMA STADI (WAWAKILISHI WA WAKULIMA VIJIJINI), MADIWANI NA MBUNGE WA JIMBO

Washiriki wa Kikao cha, “Kilimo cha Kisasa cha Mihogo ndani ya Jimbo la Musoma Vijijini.

Leo Jumatatu, tarehe 17.12.2018 KIKAO cha MATAYARISHO ya Kilimo cha KISASA cha MIHOGO ndani ya Jimbo la Musoma Vijijini kimefanyika Kijijini Maneke chini ya Uenyekiti wa Mbunge wa Jimbo Prof Dr Sospeter Muhongo
YALIYOKUBALIWA:
(1) Matayarisho haya ni ya Kilimo cha kuanzia Msimu wa Masika, Machi- Mai 2019
(2) Kilimo cha Zao la Mihogo ndani ya Jimbo (Kata 21, Vijiji 68, Vitongoji 374) liendeshwe kwa Muongozo wa Sheria Ndogo kama ilivyo kwenye Kilimo cha Pamba.
(3) Zao la Mihogo liwe zao la CHAKULA na BIASHARA kwa Jimbo la Musoma Vijijini
AGIZO:
Wataalamu wa Kilimo watawasilisha Andiko hilo kwa Baraza la Madiwani kabla ya tarehe 31.12.2018
Takwimu zinazoonyesha MAHITAJI ya WINGI wa MBEGU ziwakilishwe na Wataalamu kabla ya tarehe 30.01.2019
(4) Mbegu ya MKOMBOZI ndiyo imependekezwa na Wataalamu wa Kilimo kuwa CHAGUO la wakati huu wa MBEGU BORA Jimboni.
(5) ANDIKO LA KUELEKEZA WAKULIMA WA MIHOGO Jimboni litatolewa na Wataalamu wa Kilimo ifikapo tarehe 24.12.2018. Andiko litakuwa la Ukurasa mmoja – aina ya mbegu na upatikanaji wake, mbolea, madawa, upandaji & uvunaji, n.k.
(6) Halmashauri ITUNGE SHERIA ndogo zinazowalinda Wakulima na Wafugaji. Sheria Ndogo za kulinda Mazingira.. miti itakayopandwa nayo ilindwe na Sheria Ndogo za Halmashauri.
(7) ZANA ZA KILIMO
(a) Fursa za Mikopo ya MATREKETA IPO kwa Vyama vya Msingi vya Ushirika (AMCOS), Vikundi na Watu Binafsi. Halmashauri INASUBIRI KUWASAIDIA WAOMBAJI
(b) PLAU – Ofisi ya Mbunge INASUBIRI KUPOKEA orodha ya Vikundi vya Kilimo VINAVYOOMBA PLAU. Wenye MIFUGO ya kutumiwa kwenye Kilimo cha kutumia PLAU wawemo kwenye Vikundi hivyo.