SHULE SHIKIZI EGENGE YAKAMILIKA

JENGO la SHULE SHIKIZI EGENGE, Kijiji cha Busamba, Kata ya Etaro.

SERIKALI kupitia Halmashauri ya Wilaya ya Musoma  INAZIDI KUBORESHA MIUNDOMBIMU YA ELIMU kwenye Jimbo la Musoma Vijijini.
Shule SHIKIZI Egenge ya Kijiji cha Busamba, Kata ya Etaro IMEKAMILIKA.
Mradi wa EQUIP umetoa fedha za ujenzi na WANANCHI wamechangia NGUVU ZAO ili kupunguza gharama za ujenzi.
MAJENGO YA SHULE SHIKIZI EGENGE ni: (i) Vyumba 2 vya Madarasa, (ii) Ofisi 1 ya Walimu, (iii) Vyoo 2 (Wanafunzi 1 & Walimu 1)
Fundi Mkuu, Ndugu Metai Makamba  (kutoka Kijiji cha Lyasembe, Kata ya Murangi: Simu 0743 282 595) anakaribisha WANANCHI na Viongozi mbalimbali waende kujifunza ujenzi bora wa Miundombinu ya Shule kutoka Shule Shikizi Egenge.