BMZ WAKAMILISHA ZOEZI LA UGAWAJI WA VIFAA VYA ELIMU KWA WANAFUNZI WENYE ULEMAVU

Makabidhiano ya Vifaa vya Elimu Kutoka BMZ Kwenye Kata ya Nyamurandirira na Kiriba.

Na Fedson Masawa, Msaidizi wa Mbunge
MRADI wa BMZ (The Federal Ministry of Economic Cooperation and Development) wa UJERUMANI leo tarehe 8.11.2018 umekamilisha zoezi la Ugawaji wa Vifaa vya Elimu kwa Wanafunzi wenye Ulemavu katika Kata ya Murangi, Nyamurandirira na Kiriba zote za Jimbo la Musoma Vijijini.
Awali akizungumza na WAZAZI wa WATOTO wenye ULEMAVU, Wasaidizi wa Mbunge wa Jimbo la Musoma Vijijini, wawakilishi wa WALIMU na Viongozi wa Serikali ngazi ya Kata na Vijiji, Meneja wa BMZ Mkoa wa Mara, Bi Niwaely Sandy alizitaja Kata 10 zilizo kwenye Mradi kuwa ni Nyambono, Bugwema, Bukumi, Makojo, Bwasi, Bukima, Murangi, Nyamurandirira, Suguti na Kiriba.
Ndugu Niwaely aliendelea kuulezea Mradi huu na kusema, “Vifaa tulivyovigawa ni MADAFTARI, KALAMU na  BEGI za kubebea vifaa vya shule.
Vilevile Mradi wa BMZ umegawa T-shirt kwa Viongozi wa Kata na Wawakilishi wa Walimu kutoka Shule zilizo na Watoto wenye Ulemavu.
Mwenyekiti wa SHIVYAWATA Wilaya, Ndugu Yohana Magai alitoa pendekezo kwa Viongozi wa Serikali la kuwachukulia hatua Wazazi ambao hawataki kuandikisha shuleni watoto wenye ulemavu kwani kufanya hivyo ni kuwanyima haki yao ya msingi ya kupata elimu.
Vilevile Kiongozi huyo amewashauri Viongozi Wahusika wahakikishe MIUNDOMBINU ya MAJENGO ya Taasisi zote iwe rafiki kwa watu wenye ulemavu.
Naye Mtendaji wa Kata ya Kiriba, Bi  Pendo Isack Mwita aliwapongeza BMZ kwa kazi nzuri wanayoifanya katika Jamii na kuahidi kupambana na wazazi wote watakaokataa kuwaandikisha shuleni watoto wenye ulemavu.
Kwa upande wake Mratibu Elimu Kata ya Nyamurandirira, Ndugu Rehema Mateko alisema atahakikisha TAARIFA za Wanafunzi wenye ULEMAVU zinahifadhiwa na kuwasilishwa kwenye Mamlaka husika kwa msaada zaidi pale itakapotokea.
Aidha, mmoja wa Wanafunzi waliogawiwa Vifaa vya Elimu kutoka BMZ, Nyawaye Magesa Kamenge anayesoma Darasa la tatu katika Shule ya Msingi Nyamiyenga, Kijiji cha Kiriba, Kata ya Kiriba alishukuru kwa msaada alioupokea na kuahidi kufanya vizuri zaidi katika masomo yake.
Ofisi ya Mbunge wa Musoma Vijijini imesema itaendelea kushirikiana na BMZ kuhakikisha MRADI wao wa KUSAIDIA na KUWAWEZESHA KI- UCHUMI WALEMAVU unafanikiwa.
TUENDELEE KUWASAIDIA NA KUWAWEZESHA KI-UCHUMI WALEMAVU JIMBONI MWETU – SHUKURANI NYINGI KWA MRADI WA BMZ