PROF MUHONGO ASHIRIKI HARAMBEE UJENZI WA BWENI LA WASICHANA LA SEKONDARI YA BWASI

Viongozi mbalimbali walioshiriki katika Harambee ya kuchangia Ujenzi wa Bweni la Wasichana katika Shule ya Sekondari Bwasi

Na Verediana Mugoma, Msaidizi wa Mbunge
OFISI ya Mbunge wa Jimbo la Musoma Vijijini imekabidhi mchango SARUJI MIFUKO  50 ya kutoka kwa Mbunge wa Jimbo hilo Prof Sospeter Muhongo kwa ajili ya kuchangia ukarabati wa Bweni la Wasichana katika Shule ya Sekondari Bwasi iliyopo Kijijini Bwasi, Kata ya Bwasi.
Akizungumza kabla ya kukabidhi Mchango huo kwa niaba ya Mbunge, Msaidizi wa Mbunge Verediana Mgoma alisema,
“Ili kuharakisha shughuli za maendeleo Jimboni, WANANCHI VIJIJINI, WADAU WA MAENDELEO,  WAZAWA wa Jimbo la Musoma Vijijini na RAFIKI ZAO hawana budi kujitolea na  kushiriki kikamilifu kuchangia MAENDELEO YA VIJIJI VYETU kwa KUSHIRIKIANA na SERIKALI, Madiwani na Mbunge wa Jimbo  kufikia malengo yaliyowekwa kwa wakati.”
Naye Mgeni Rasmi katika Harambee hiyo Dr. Fredy J. Gamba, amemshukuru Prof Muhongo kwa kuipa kipaumbele Sekta ya Elimu na kusema kama WANANCHI wataungana pamoja na kumuunga mkono Mbunge, Musoma Vijijini itapiga hatua nzuri ya maendeleo ya Elimu na itakuwa ya mfano wa kuigwa.
Kwa upande wake Mkuu wa Shule ya Sekondari ya Bwasi Ibrahim Chacha ametoa shukrani zake za dhati kwa WACHANGIAJI WOTE walioshiriki katika kufanikisha HARAMBEE hiyo na kuahidi kuitumia SARUJI iliyotoka kwa Mbunge ndani ya kipindi kifupi kama ulivyo utaratibu wa matumizi ya vifaa vinavyotoka kwa Mbunge wa Jimbo.
Sekondari ya Bwasi imeishapokea VITABU VYA MASOMO YA SEKONDARI kutoka kwa Mbunge Prof Muhongo. Vitabu hivyo vinatoka USA na UK. January 2019, Mbunge amepanga kugawa vitabu kwa mara ya nne (4) kwa Shule zote za Sekondari na Msingi za Jimboni.
JIMBO LA MUSOMA VIJIJINI – QUALITY EDUCATION AT ALL LEVELS