KASI YA UBORESHAJI WA MIUNDOMBINU YA ELIMU JIMBONI YAONGEZEKA

Wananchi wakishiriki katika kazi ya kujaza kifusi kwenye Msingi wa SHULE MPYA ya MSINGI YA BUANGA

Na Verediana Mgoma, Msaidizi wa Mbunge
WANANCHI WA KIJIJI  CHA BUANGA WAANZA UJENZI WA SHULE MPYA
Wananchi wa Kijiji cha Buanga, Kata ya Rusoli WAMEAMUA KUJITOLEA kujenga Vyumba Vinne (4) vya MADARASA katika Shule  Mpya ya Msingi inayojengwa katika Kitongoji cha Chilugwe ili kuwapunguzia UMBALI WATOTO WANAOTEMBEA WA takribani Km 5 kwenda masomoni kwenye Shule ya Msingi Bwenda.
Ujenzi wa Shule Mpya katika Kijiji cha Buanga, ni hatua muhimu katika  KUINUA KIWANGO cha UBORA WA ELIMU itolewayo kwenye Kata ya Rusoli. WANAFUNZI  ambao wengi wao wamelazimika kukatisha masomo yao na wengine kuwa watoro sugu shuleni, SASA WAMEKUWA NA MATUMAINI MAPYA KIELIMU.
Awali wakizungumza na Mwandishi wa Habari hizi Kijijini Buanga, WANANCHI  hao wameeleza kwa namna ambavyo wamewiwa kwa kutoa maeneo yao, kuuza mifugo yao kwa ajili ya ujenzi wa SHULE hiyo MPYA ili kuokoa na kuinua taaluma kwa WATOTO WAO hasa wenye umri wa kuanza SHULE, likiwemo DARASA la AWALI.
Akitoa taarifa ya ujenzi huo, Mtendaji wa Kijiji cha Buanga,  Ndugu Tumaini Rugembe, ameeleza kwamba, “umbali umekuwa kisababishi cha watoto wao kupotea, na kutofika shuleni kwa muda muafaka.”  Aliongezea kuwa hadi kufikia January 2019, wanatarajia SHULE hiyo iwe IMEFUNGULIWA.”
Diwani wa Kata ya Rusoli, Mhe Boazi M. Nyeura kwa niaba ya wananchi wake amesema kuwa, ANAUTAMBUA MCHANGO mkubwa wa SERIKALI na VIONGOZI mbalimbali ikiwa ni pamoja na Mbunge Prof Sospeter Muhongo kwa mchango wake wa MADAWATI 162 katika Shule ya Msingi Bwenda A na B, SARUJI MIFUKO 120 na MABATI 50.
MFUKO WA JIMBO ulichangia MABATI 54 na Halmashauri ilichangia Shilingi Milioni 5 kwa ajili ya ukamilishaji wa Vyumba Vinne (4) vya Madarasa katika Shule ya Bwenda A na B, Kijijini Buanga.
Aidha Diwani alimpongeza Mkuu wa Wilaya(DC) Dr. Vincent Naano Anney  kwa UHAMASISHAJI wake kwa WANANCHI ili kuwezesha ujenzi wa Vyumba vya MADARASA na MAABARA ndani ya Kata ya Rusoli.
Mhe Diwani  Boazi Nyeura AMEENDELEA KUWAOMBA WADAU WA MAENDELEO WAJITOKEZE kushirikiana na Wananchi wa Kata ya Rusoli KUBORESHA MIUNDOMBINU ya ELIMU na AFYA NDANI YA KATA HIYO.