UJENZI WA SHULE YA SEKONDARI BUSAMBARA WAENDELEA KWA KASI KUBWA 

WANANCHI WA KATA YA BUSAMBARA (Vijiji vya Maneke, Kwikuba na Mwiringo) Wakijitolea kusomba mchanga, mawe, kokoto, kufyatua tofali, kusomba maji ili kumsaidia Fundi ujenzi.

Na Hamisa Gamba Msaidizi wa Mbunge
Hivi karibuni WANANCHI wa Kata ya Busambara, Jimboni Musoma Vijijini WAMEAMUA KWA KAULI MOJA KUONGEZA KASI YA Ujenzi wa Vyumba Vipya vya Madarasa ya Shule Mpya ya Sekondari Busambara baada ya kuwa umesimama kwa muda.
Hatua hii ilifikiwa baada ya Mbunge wa Jimbo hilo, Prof Sospeter Muhongo kuwatembelea wananchi wa Kata hiyo ya  Busambara na KUWAHAMASISHA kuendelea na Ujenzi na Kuukamilisha ifikapo Disemba 2018 kama ILIVYOKUSUDIWA.
Tarehe 14/7/2018, Mbunge wa Jimbo, Prof Muhongo aliwakabidhi Wananchi wa Kijiji cha Kwikuba Saruji Mifuko 50 baada ya Kijiji hicho KUONYESHA ARI KUBWA YA KUKAMILISHA kwa wakati Vyumba vya Madarasa ilivyopangiwa. Saruji ilinunuliwa Kijijini Kwikuba.
Wakiendelea kufanya jitihada za Ujenzi wa Madarasa, tarehe 23/7/2018 Msaidizi wa Mbunge aliwatembelea Wananchi hao wa kutoka Vijiji 3 wakiwa katika majukumu yao kadri walivyojipangia na kukuta yafuatayo:
(1) Kijiji cha Kwikuba:
– Wananchi walikuwa katika hatua za ukamilishaji wa Msingi wa Vyumba viwili vya Madarasa.
(2) Kijiji cha Maneke:
– Wananchi walikuwa katika ufyatuaji wa matofali.
(3) Kijiji cha Mwiringo:
– Wananchi walikuwa wakisomba mchanga wa kufyatua matofali. Kazi ilipangwa kuanza Jumatano, tarehe 25/7/2018.
Kutokana na MAKUBALIANO YA MBUNGE na WANANCHI wa Vijiji vya Maneke na Mwiringo kuendelea na ujenzi kuanzia tarehe 25.07.2018, Mbunge wa Jimbo Prof Muhongo ALITIMIZA AHADI YAKE ya KUCHANGIA Saruji Mifuko 50 kwa kila Kijiji, na saruji imenunuliwa Kijijini  Kwikuba.
WANANCHI WA KATA YA BUSAMBARA (Vijiji vya Maneke, Kwikuba na Mwiringo) WAMEKUBALI KUJITOLEA KUSOMBA mchanga, mawe, kokoto, kufyatua tofali, kusomba maji na kumsaidia Fundi ujenzi. WANAOMBA MCHANGO WAKO WAKAMILISHE UJENZI WA SHULE YA SEKONDARI BUSAMBARA.
Mchango wako uwakilishwe kwa Serikali ya Kijiji cha Maneke, Kwikuba na Mwiringo. Ikishindikana Wasiliana na Msaidizi wa Mbunge wa eneo hilo:
Simu:
   0762 626 881