SHEREHE ZA UZINDUZI WA SHULE YA MSINGI NYEGINA B, KIJIJI CHA NYEGINA

Tarehe 15.07.2018, Mbunge Prof Sospeter Muhongo (Mgeni Rasmi) na Viongozi wa Vyama vya Siasa (CCM, CHADEMA, ACT) na Serikali walishiriki Sherehe za Uzinduzi wa S/M Nyegina B.

Jumapili, 15.07.2018,  Sherehe za Kuzindua S/M Nyegina B zilifana sana.
Kijiji cha Nyegina, Kata ya Nyegina, Musoma Vijijini,  kinayo historia nzuri ya  ELIMU na MAENDELEO.
Shule ya Msingi Nyegina ya Kanisa la Katoliki ilijengwa Mwaka 1928 na Darasa la Kwanza lilianzishwa Mwaka 1930. Kanisa la Katoliki lilijengwa Kijijini hapo Mwaka 1911.
Kijiji cha Nyegina kimekuwa KITOVU CHA ELIMU kwani kuna Shule ya Msingi, Sekondari na High School. Kuna Maktaba ya kisasa na Kituo cha TEHAMA kinaendelea kupanuliwa hapo Kijijini. Mbunge wa Jimbo Prof Sospeter Muhongo amegawia MAKTABA hiyo VITABU alivyopewa kutoka Marekani na Uingereza. Baba Paroko Kazeri ni Kiongozi Mahiri wa masuala ya Elimu, Afya, Kilimo, Mazingira, TEHAMA  na Maendeleo ndani ya Jimbo la Musoma Vijijini.
Jumapili, 15.07.2018, Mbunge Prof Sospeter Muhongo (Mgeni Rasmi) na Viongozi wa Vyama vya Siasa (CCM, CHADEMA, ACT) na Serikali walishiriki Sherehe za Uzinduzi wa S/M Nyegina B.
CCM iliwakilishwa na M/Kiti Wilaya (Ndg Nyabukika), Katibu Wilaya (Ndg Koyo) na Kaimu K/Wilaya Wazazi (Ndg Lucia John). M/Kiti wa Halmashauri (Ndg Magoma),  Diwani wa Kata hiyo, Ndugu Majira, na Wafanyakazi wa Halmashauri waliungana na Wananchi wa Kijiji cha Nyegina, na Waalikwa mbalimbali kwenye UZINDUZI huo.
HARAMBEE ilipigwa ya KUCHANGIA UJENZI wa Vyumba vingine vya Madarasa vya Shule hiyo. Saruji Mifuko 215 na Fedha Tshs 495,000 vilichangwa kwenye HARAMBEE hiyo. Mbunge Prof Muhongo alichangia, kwa awamu hiyo ya ujenzi, Saruji Mifuko 50 iliyonunuliwa Kijiji cha jirani cha Etaro.
Shirika la EQUIP la Uingereza na Kanisa la Angalikani la Marekani nao WANACHANGIA ujenzi wa Shule ya Msingi Nyegina B.
Picha hapo chini zinaonyesha KILELE CHA SHEREHE ZA UFUNGUZI wa Shule ya Msingi Nyegina B.
UJENZI UNAENDELEA TUNAOMBA SANA MCHANGO WAKO. WANAVIJIJI WAMEAMUA KUSHIRIKIANA NA SERIKALI KUCHANGIA MAENDELEA YAO TUWAUNGE MKONO.