UJENZI NA UBORESHAJI WA MIUNDOMBINU YA ELIMU JIMBONI

 

Mbunge wa Jimbo la Musoma Vijijini akishirikiana na Mwenyekiti wa CCM wa Wilaya ya Musoma Vijijini, Ndugu Nyabukika KUHAMASISHA ujenzi wa Vyumba vya Madarasa vya Shule za Msingi na Sekondari Jimboni mwao

Jumamosi, 14.07.2018, Mbunge wa Jimbo la Musoma Vijijini alishirikiana na Mwenyekiti wa CCM wa Wilaya ya Musoma Vijijini, Ndugu Nyabukika KUHAMASISHA ujenzi wa Vyumba vya Madarasa vya Shule za Msingi na Sekondari Jimboni mwao. Katibu wa CCM Wilaya Ndg Koyo na Mjumbe wa Kamati ya Siasa Ndg Mwalimu Kerenge walishiriki kwenye ziara hiyo ya UHAMASISHAJI wa uboreshaji wa miundombinu ya Elimu kwenye Jimbo la Musoma Vijijini.

(1) SHULE MPYA YA MSINGI YA MWIKOKO, Kijiji cha Chitare, Kata ya Makojo: Picha Namba 1-4 hapo chini zinaonyesha Mkutano wa Wanakijiji wa Chitare wakishiriki HARAMBEE ya kuchangia ujenzi wa Vyumba Vipya vya Madarasa ya Shule hiyo ya Msingi. Kwa awamu hii ya ujenzi, Mbunge Prof Muhongo amechangia Saruji Mifuko 5O iliyonunuliwa Kijiji jirani cha Bukima.

(2) SEKONDARI YA KATA YA USAMBARA: Kata hii yenye Vijiji 3 (Maneke, Kwikuba na Mwiringo) haina Sekondari.

Wananchi wa Kata ya Busambara WAMEAMUA KWAMBA IFIKAPO JANUARI 2019 Sekondari hiyo iwe IMEKAMILIKA na kuanza kutoa elimu.

Wananchi wamepiga HARAMBEE kwa kutoa fedha taslimu na vifaa vya ujenzi. Mbunge Prof Muhongo, amechangia Saruji Mifuko 50 iliyonunuliwa Kijijini hapo. Michango mingine atatoa baada ya KURIDHIKA na KASI ya ushiriki wa Vijiji vya Maneke na Mwiringo kwenye ujenzi wa Sekondari hii. Ushiriki wa Vijiji hivi viwili kwa sasa ni hafifu.

Picha Namba 5-8 zinaonyesha Mkutano wa Wananchi wa Kata ya Busambara wakishiriki kwenye HARAMBEE ya ujenzi wa Sekondari ya Kata yao.

Wananchi wa Vijiji vya CHITARE (Kata ya Makojo), na KWIKUBA, MWIRINGO na MANEKE (Kata ya Busambara) wanaomba MCHANGO WAKO UWASAIDIE ujenzi wa shule zao ambazo WAMEAMUA KUZIJENGA KWA KUJITOLEA na kwa kushirikiana na Serikali.