KILIMO CHA MVUA ZA VULI

JIMBO LA MUSOMA VIJIJINI – TUJITAYARISHE KWA KILIMO CHA MVUA ZA VULI

Wataalamu wetu wa Halmashauri ya Wilaya ya Musoma WANATUSHAURI hivi:

KILIMO cha MTAMA, MIHOGO na MAHINDI cha Msimu wa Vuli huanza mwishoni mwa Mwezi SEPTEMBA, na kuendelea hadi OKTOBA na NOVEMBA.

MBEGU ZINAZOHITAJIKA

Kiasi cha MBEGU kinachohitajika
(1) Mahindi: Kilo 82,500 kwa Ekari 20,625
(2) Mtama: Kilo 21,000 kwa Ekari 7,000
(3) Mihogo: Pingili 78,000,000 kwa Ekari 19,500

BEI ZA MBEGU (ASA MOROGORO)

(1) Mtama: Tshs 2,300 kwa kilo moja
(2) Mahindi: Tshs 2, 300 kwa kilo moja
(3) Vijiti Vya Mihogo: Tshs 200,000 vinavyotosha ekari moja

Ndugu zangu MADIWANI, HALMASHAURI, MKUU WA WILAYA, MBUNGE wa JIMBO, na WADAU wa MAENDELEO YA MUSOMA VIJIJINI tunaombwa tujitayarishe KUZIPATA MBEGU HIZI KWA WAKULIMA JIMBONI KWENYE MWEZI AGOSTI 2018 (mbegu kuanza kugawiwa Jimboni katikati mwa Agosti 2018).

Nashauri tufanye Kikao tarehe 10 Julai 2018 Ofisini kwa DC wa Musoma kujadili na kuweka bayana namna ya kuzipata mbegu hizo.

Je Wanavijiji wauziwe mbegu au Wanavijiji wapewe mkopo wa mbegu hizo au Wanavijiji wasaidiwe kwa kugawiwa mbegu hizo bure kutokana na uchumi wao kuwa hafifu.