WANANCHI WAMEKUA NA MWITIKIO MKUBWA WA KUJITUMA NA KUJITOLEA KUHARAKISHA UPATIKANAJI WA MAENDELEO YAO

Mbunge wa Musoma Vijijini, akifuatana wa Viongozi wa Wilaya wa CCM (Katibu wa CCM, Katibu wa WAZAZI na Katibu wa UVCCM) kukagua MIRADI YA UJENZI inayotekelezwa Jimboni humo.

Jumatano, 13.06.2018, Mbunge wa Musoma Vijijini, akifuatana wa Viongozi wa Wilaya wa CCM (Katibu wa CCM, Katibu wa WAZAZI na Katibu wa UVCCM) wamekagua MIRADI YA UJENZI inayotekelezwa Jimboni humo kwa wakati huu.

Kijiji cha Bukima kimeamua KUPANUA ZAHANATI YAKE kwa kuongeza Jengo lenye WADI 3 (Wadi ya Wazazi, Watoto & Akina Mama, na Wadi ya Wanaume). Picha za kwanza 3 zinaonyesha eneo la ujenzi huo. Mbunge wa Musoma Vijijini amechangia Saruji Mifuko 100 na wananchi wanaendelea kuchangia saruji, kusomba mawe, mchanga, n.k.

Kijiji cha Saragana wameamua kujenga KITUO CHA POLISI kitakachohudumia Kata zaidi ya 2. Wananchi wamejitolea kusomba mchanga na maji ya kufyatua tofali zaidi ya 4,000. Polisi Wilaya (OCD) imechangia Saruji Mifuko 60 na leo Mbunge wa Jimbo, Prof Sospeter amechangia Saruji Mifuko 100. Picha namba 4 na 5 hapo chini zinaonyesha tukio hilo Kijijini Saragana.

Kijiji cha Nyambono kimekubali KUSHIRIKIANA na Wazaliwa wa Kijiji hicho (Wafadhili) kujenga KITUO CHA AFYA. Wiki hii wanamaliza ujenzi wa msingi wa Jengo la Matibabu. Mbunge wa Jimbo, Prof Sospeter Muhongo amechangia Saruji Mifuko 100. Picha 2 za mwisho zinaonyesha msingi unaojengwa.

Wananchi wa Vijiji vyote 68 vya Jimbo la Musoma Vijijini wamekuwa na hamasa ya KUJITOLEA kuharakisha Ujenzi na Uboreshaji wa Miundombinu ya Elimu na Afya vijijini mwao kwa kushirikiana na Serikali.