MABARAZA YA WAZEE WA USHAURI, USHAWISHI NA MAADILI

Na Fedson Masawa, Msaidizi wa Mbunge

PROF. MUHONGO AZINDUA MABARAZA YA WAZEE WA USHAURI, USHAWISHI NA MAADILI

Wazee wa mabaraza ya kata 21 za jimbo la Musoma vijijini wakiwa kwenye kikao cha uzinduzi wa mabaraza yao uliotekelezwa na Mbunge wa Jimbo holi Prof. Muhongo (hayupo katika picha)

Mbunge wa Jimbo la Musoma Vijijini Prof Sospeter Muhongo leo April 30 amefanya uzinduzi wa mabaraza ya wazee wa ushauri na maadili ngazi ya kata kwa kata zote 21 za Jimbo hilo.

Akizungumza na wazee wakati wa uzinduzi wa mabaraza hayo kijijini Chumwi, Prof Muhongo amewaeleza wazee hao kuwa majukumu yao makubwa ni kutoa ushauri na kuhamasisha shughuli za maendeeo bila kuingilia miimili ya serikali za vijiji, kata n.k ili kuharakisha mafanikio chanya Jimboni.

Kwa upande wao wazee kutoka kata 21 za Jimbo la Musom vijijini wameungana pamoja kuhakikisha wanasimamia majukumu yao ya ushawishi, ushauri na uhamasishi katika mendeleo na uchumi hasa Elimu, Afya na Kilimo vikiwa ni vipaumbele vya Jimbohilo.

“Tutahakikisha Elimu, Afya na Kilimo ndio itakuwa nguzo ya kuinua uchumi na maendeleo ya Jimbo letu” alisema mzee Chriphod Nyaturo kwa niaba ya wazee wa hao.

Hii ni mara ya pili Prof Muhongo akizindua mabaraza ya wazee ambapo kwa mara ya kwanza alizindua mabaraza ya wazee ngazi ya vijiji  mwishoni mwa mwezi Machi 2018, lengo likiwa ni kuimarisha nguvu ya ushawishi na uhamasishaji wa shughuli za maendeleo na uchumi Jimboni.

Kwa upande mwingine,  Mbunge wa Jimbo la Musoma Vijijini amefanya Kikao na Wenyeviti wa CCM wa Kata za Jimbo lake wakijadili juu ya usimamiaji wao wa utekelezaji wa Miradi ya Uchumi na Maendeleo (Ilani ya CCM ya Uchaguzi)  kwenye Kata zao.