WANAWAKE WATAKIWA KUUNDA VIKUNDI VYA MAENDELEO

Na Hamisa Gamba

MWENYEKITI wa Umoja wa Wanawake wa Chama cha Mapinduzi CCM (UWT) Mkoani Mara, Wegesa Hassan amewataka wanawake mkoani humo kuunda vikundi ili kufanya miradi mbalimbali itakayowaletea maendeleo.

Wegesa alitoa wito huo kwenye kikao cha Jumuiya hiyo kilichofanyika Murangi, kwa lengo la kuhamasisha mshikamano na suala la maendeleo, ambapo aliwataka wanawake kuachana na makundi yasiyo na tija ndani ya Jumuiya yao.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa UWT Musoma vijijini Abia Masaule kwa niaba ya wajumbe wake, ametoa shukrani kwa Mbunge wa Jimbo la Musoma vijijini Prof. Sospeter Muhongo kwa umoja alioonesha na kuungana na wanawake hao katika kuwezesha kikao hicho kilichofanyika Machi 21, 2018.