KILIMO CHA ALIZETI NA UFUTA JIMBO LA MUSOMA VIJIJINI

Wakulima wa Jimbo Musoma Vijijini wameendelea kupata uzoefu wa kulima ALIZETI na kwa sasa wanaingia msimu wa 3. Mbunge wa Musoma Vijijini, DC, DED na Afisa Kilimo wa Halmashauri wamefanya Kikao leo tarehe 25 Jan 2018 kukamilisha utaratibu wa upatikanaji wa mbegu za ALIZETI na UFUTA kwa ajili ya kilimo cha mazao hayo kwa msimu huu mpya.

Viongozi hao wamekubaliana kununua mbegu za ALIZETI kilo 4,974 zitakazonunuliwa na Mbunge wa Jimbo (Prof Sospeter Muhongo), na kilo 2,651 za UFUTA zitakazonunuliwa na Halmashauri. Imeazimiwa kwamba mbegu zote hizo zipatikane na kuwafikia Wakulima Jimboni kuanzia tarehe 10 Feb 2018. Jimbo la Musoma Vijijini limeazimia kuwa na ukulima mkubwa wa mazao ya PAMBA, ALIZETI, UFUTA, MUHOGO na mazao mengine ya chakula.

Ofisi ya Mbunge
www.musomavijijini.or.tz