HARAMBEE YA UJENZI WA SHULE SHIKIZI KIUNDA, MUSOMA VIJIJINI

Hatua iliyofikiwa kwenye ujenzi wa miundombinu ya elimu kwenye Shule Shikizi Kiunda ya Kijijini Kamguruki, Musoma Vijijini.

Tarehe:
Ijumaa, 12.1.2024
Saa 8 mchana

Mahali:
Kitongoji cha Kiunda
Kijijini Kamguruki

Akaunti ya Benki:
Benki: NMB
Akaunti Na: 30302300679
Jina la Akaunti: Kijiji cha Kamguruki

Taarifa ya Kiunda:
Shule Shikizi Kiunda inajengwa kwenye Kitongoji cha Kiunda, Kijijini Kamguruki, Kata ya Nyakatende.

Shule hii inatayarisha watoto wa vitongoji 3 kwenye masomo ya awali, baadae watoto hao wanaenda kuanza masomo ya Shule ya Msingi mbali na nyumbani kwao - tatizo la umbali mrefu wa kwenda masomoni.

Ujenzi wa Shule Shikizi Kiunda:
Wote tunakarabishwa kuchangia ujenzi wa shule hii kwa kushiriki HARAMBEE iliyoelezwa hapo juu, au kutuma mchango wako moja kwa moja kwenye Akaunti ya Kijiji cha Kamguruki.

Picha ya hapa inaonesha hatua iliyofikiwa kwenye ujenzi wa miundombinu ya elimu kwenye Shule Shikizi Kiunda ya Kijijini Kamguruki, Musoma Vijijini.

KARIBU TUBORESHE ELIMU VIJIJINI MWETU

Ofisi ya Mbunge
Jimbo la Musoma Vijijini
www.musomavijijini.or.tz

Tarehe:
Jumamosi, 6.1.2024