KILIMO CHA UMWAGILIAJI NDANI YA BONDE LA BUGWEMA

Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere alidhamiria kujenga miundombinu ya kilimo cha umwagiliaji kwenye bonde la Bugwema lililoko Musoma Vijijini.

Ujenzi wa miundombinu ya kilimo cha umwagiliaji ilianza kujengwa Mwaka 1974. Mradi ukasimama.

Mbunge wa Jimbo la Musoma Vijijini, Prof Sospeter Muhongo, ameiomba Serikali yetu ifufue mradi huo. Serikali imekubali na kwenye Bajeti ya Mwaka huu wa Fedha (2023/2024) - kazi za, "feasibility studies & designing", zimeanza.

Jimbo letu lina mabombe makubwa mawili yenye vigezo vyote vya uanzishwaji wa kilimo kikubwa cha umwagiliaji - hayo ni mabonde ya Bugwema & Suguti.

KILIMO CHA UMWAGILIAJI NDIYO SULUHISHO LA UHAKIKA KWA UPATIKANAJI WA CHAKULA CHA KUTOSHA & CHA BEI NAFUU NCHINI MWETU!

Tafadhali sikiliza CLIP/VIDEO kutoka Kijijini Bugwema - imeambatanishwa hapa.

Tafadhali usiache kutembelea TOVUTI ya Jimbo letu ambayo ni:
www.musomavijijini.or.tz

Ofisi ya Mbunge
Jimbo la Musoma Vijijini
www.musomavijijini.or.tz

Tarehe:
Alhamisi, 5.10.2023