Sehemu ya uharibifu uliofanyika kwenye Mwalo wa Kijiji cha Busekera, Kata ya Bukumi, Musoma Vijijini

Upepo wenye kasi kubwa na mvua kubwa vilisababisha kuwepo kwa dhoruba kubwa ndani ya Ziwa Victoria juzi tarehe 20.3.2023.

Mialo ya Musoma Vijijini ilikumbwa na dhoruba hiyo na uharibifu mkubwa umefanyika.

Tunaomba tushirikiane kuwachangia wavuvi wetu walioathirika na janga hili.

TATHMINI YA UHARIBIFU

(1) Mitumbwi ya Mwalo wa Kijiji cha Busekera
*Iliyoharibika: 137
*Inayotengenezeka: 108
*Isiyotengenezeka: 29
*Makokoro ya dagaa yaliyoharibika: 29

(2) Mitumbwi ya Mwalo wa Kijiji cha Buira
*Iliyoharibika: 39
*Inayotengenezeka: 29
*Isiyotengenezeka: 10
*Makokoro ya dagaa yaliyoharibiwa: 15

(3) Mitumbwi ya Mwalo wa Kijiji cha Bwai Kumsoma
*Iliyoharibika: 25
*Inayotengenezeka: 21
*Isiyotengenezeka: 4
*Makokoro ya dagaa yaliyoharibika: 15

(4) Mitumbwi ya Mwalo wa Kijiji cha Kasoma
*Iliyoharibika: 10
*Inayotengenezeka:9
*Isiyotengenezeka:1
*Makokoro ya dagaa yaliyoharibika: 3

GHARAMA ZA MATENGENEZO
Mifano ya hapa chini itakupatia picha unayoweza kuitumia kutoa mchango wako.

(1) Gharama za kutengeneza Mtumbwi
*Tsh 1,700,000
*Ubao 1 wa 9"x10"
Tsh 12,000

(2) Gharama za kutengeneza Kokoro la Dagaa
*Tsh 1,400,000

UWASILISHAJI WA MCHANGO WAKO

Tafadhali mpelekee:
DC Wilaya ya Musoma
Simu: 0756 088 624

Michango ya awali:
*Tungalipenda kuanza kuwasilisha michango yetu ya awali kwa wavuvi waathirika siku ya Alhamisi, 30.3.2023

Ofisi ya Mbunge
Jimbo la Musoma Vijijini
www.musomavijijini.or.tz

Tarehe:
Jumatano, 22.3.2023