HARAMBEE ZA MBUNGE WA JIMBO: SARUJI INAENDELEA KUTOLEWA

Viongozi kutoka Muhoji Sekondari wakipokea Saruji Mifuko 50

Jumatano, 25.1.2023, Mbunge wa Jimbo la Musoma Vijijini, Prof Sospeter Muhongo alitoa SARUJI MIFUKO 50 kuchangia ujenzi wa Sekondari mpya ya Kijijini Muhoji, Kata ya Bugwema.

Hiyo ni sehemu ya SARUJI MIFUKO 150 aliyoahidi kwenye HARAMBEE ya jana yake ya kuchangia Muhoji Sekondari.

Viongozi kutoka Muhoji Sekondari walikuwepo kupokea Saruji Mifuko 50.

Hii ni Sekondari ya pili ya Kata ya Bugwema

pia Mbunge huyo aliipatia Bwai Sekondari SARUJI MIFUKO 50 na MABATI BUNDLE 2 (mabati 24) Hii ni matokeo ya HARAMBEE ya tarehe 19.1.2023.

Bwai Sekondari ikimaliza hiyo Mifuko 50, itapewa Mifuko mingine 50. Ahadi ya Mbunge huyo ni kuchangia jumla ya Saruji Mifuko 100.

Hii ni Sekondari ya pili ya Kata ya Kiriba

KARIBUNI TUCHANGIE KWA VITENDO UJENZI NA UBORESHAJI WA SHULE ZETU

Ofisi ya Mbunge
Jimbo la Musoma Vijijini
www.musomavijijini.or.tz

Tarehe:
Jumatano, 25.1.2023