JIMBO LA MUSOMA VIJIJINI LAFURAHISHWA KUWEPO KWA FEDHA ZA IMF KWA AJILI YA KUKAMILISHA UJENZI WA SHULE SHIKIZI

Baadhi ya majengo yaliyokamilika katika SHULE Shikizi NYASAENGE, Kijijini Kataryo Kata ya Tegeruka

Na: Wasaidizi wa Mbunge
*Verediana Mgoma
*Fedson Masawa
*Hamisa Gamba
*Vaileth Peter
SHULE SHIKIZI zinazojengwa na baadae kupanuliwa kuwa SHULE za MSINGI kamili zitakazojitegemea ni kumi na mbili (12). SHULE hizo ni:
1. *SHULE SHIKIZI BINYAGO* : KIJIJI CHA KABEGI, KATA YA IFULIFU
2.*SHULE SHIKIZI BUANGA*:  KIJIJI CHA BUANGA, KATA YA RUSOLI
3. *SHULE SHIKIZI BURAGA* : KIJIJI CHA BURAGA, KATA YA BUKUMI
4. *SHULE SHIKIZI EGENGE* : KIJIJI CHA BUSAMBA, KATA YA ETARO
5. *SHULE SHIKIZI GOMORA* :  KIJIJI CHA MUSANJA, KATA YA MUSANJA
6.*SHULE SHIKIZI KAGURU*:   KIJIJI CHA BUGWEMA, KATA YA BUGWEMA
7. *SHULE SHIKIZI KARUSENYI*:  KIJIJI CHA MIKUYU, KATA YA NYAMRANDIRIRA
8. *SHULE SHIKIZI  KIHUNDA*:  KIJIJI CHA KAMGURUKI, KATA YA NYAKATENDE
9.*SHULE SHIKIZI   MWIKOKO*:   KIJIJI CHA CHITARE, KATA YA MAKOJO
10. *SHULE SHIKIZI  NYASAENGE* :   KIJIJI CHA KATARYO, KATA YA TEGERUKA
11.*SHULE SHIKIZI RWANGA*: KIJIJI CHA KASOMA, KATA YA NYAMRANDIRIRA
12.*SHULE SHIKIZI   ZIWA* : KIJIJI CHA MWIRINGO, KATA YA BUSAMBARA
*WACHANGIAJI WA UJENZI WA SHULE SHIKIZI NDANI YA JIMBO LETU*
*SERIKALI KUU*
*Wananchi wa Jimbo la Musoma Vijijini wanashukiru sana kwa kupokea MICHANGO MINGI kutoka SERIKALI KUU (k.m. TAMISEMI) kwa ajili ya UJENZI na UBORESHAJI WA MIUNDOMBINU ya ELIMU kwenye shule zetu zote za Jimboni mwetu.
*WANANCHI*
*huchangia NGUVUKAZI za kusomba mawe, kokoto, mchanga na maji ya ujenzi
*Vilevile, huchangia fedha taslimu kutoka kila kaya
*MADIWANI*
*Madiwani wanashirikiana na Wanavijiji kuchangia Miradi ya ujenzi iliyoko kwenye Kata zao.
*MBUNGE WA JIMBO*
*Prof Sospeter Muhongo, Mbunge wa Jimbo la Musoma Vijijini ni mchangiaji mkubwa wa UJENZI na UBORESHAJi wa Miundombinu ya Elimu kwenye SHULE zote SHIKIZI, MSINGI na SEKONDARI za Jimboni mwetu.
*MFUKO WA JIMBO*
*Iliamuliwa kwamba Fedha za Mfuko wa Jimbo, chini ya Mwenyekiti wake, Mbunge wa Jimbo, zitumike kwenye Miradi ya ujenzi na uboreshaji wa Miundombinu ya Elimu ya shule zetu. Hayupo anayepewa fedha mkononi. Halmashauri hununua Vifaa vya ujenzi na kuvigawa kama ilivyopangwa.
*WAZALIWA WA MUSOMA VIJIJINI*
*Baadhi yao huchangia Miradi ya ujenzi ya Vijijini kwao. Majina yao hutajwa kwenye Ripoti za Ofisi ya Mbunge.
*WADAU WENGINE WA MAENDELEO*
*Jimbo letu linashukuru sana kupata WADAU wa MAENDELEO (k.m. Benki za nchini mwetu, PCI Tanzania, BMZ Ujerumani) ambao wanachangia ujenzi na uboreshaji wa Miundombinu ya Elimu ya shule zetu. Na wao pia majina yao hutajwa kwenye Ripoti za Ofisi ya Mbunge
*HALMASHAURI YETU*
*Ushauri umetolewa kwa Halmashauri yetu  ICHANGIE IPASAVYO, na kwa UWAZI, kwenye Miradi ya Maendeleo ya Wanavijiji wa Jimboni mwetu.
*JIMBO LA MUSOMA VIJIJINI LIKO TAYARI KUANZA KUTUMIA FEDHA ZA IMF*
*MAKUSUDIO ya matumizi ya FEDHA za IMF yanaoana vizuri sana na MIRADI inayotekelezwa kwa sasa Jimboni mwetu.
TUNAJENGA SHULE SHIKIZI 12, ambazo zimetajwa hapo juu na  tunatoa hapa MIFANO MIWILI kushawishi FEDHA za IMF zichangie Miradi yetu ya ujenzi wa SHULE SHIKIZI za Jimboni mwetu
SHULE SHIKIZI NYASAENGE, KIJIJINI KATARYO, KATA YA TEGERUKA
*Hapo awali, Wanafunzi wa Kitongoji cha Nyasaenge  walilazimika kutembea umbali wa zaidi ya Kilometa 10 kwenda masomoni kwenye Shule za Msingi za KATARYO na KATARYO B.
SHULE SHIKIZI hii imekamilisha Vyumba vipya 2 vya Madarasa na Ofisi 1 ya Walimu. Darasa la Awali lina Wanafunzi 106. Ujenzi unaendelea.
SHULE SHIKIZI GOMORA, KIJIJINI MUSANJA, KATA YA MUSANJA
*Tafadhali angalia PICHA zilizoko hapa zenye Jina la GOMORA.
Wanafunzi wa Kitongoji cha GOMORA wanalazimika kwenda masomoni kwenye Shule za Msingi jirani za Lyasembe (Kata ya Murangi), na  Bwenda (Kata ya Rusoli). Ujenzi wa SHULE SHIKIZI GOMORA unaendelea.
UPATIKANAJI WA FEDHA ZA IMF: PONGEZI NYINGI SANA ZINATOLEWA KWENYE SERIKALI YETU CHINI YA UONGOZI MZURI WA MHE RAIS SAMIA SULUHU HASSAN
Ofisi ya Mbunge
Jimbo la Musoma Vijijini