TARURA WILAYA YA MUSOMA YAENDELEA KUKAMILISHA MIRADI YA MWAKA WA FEDHA 2020/2021

Daraja la Chuma lililojengwa juu ya Mto Suguti kwenye Barabara ya Wanyere-Suguti.

Tarehe 16.7.2021
Jimbo la Musoma Vijijini
BARABARA YA WANYERE – KATARYO
*DARAJA LA CHUMA
Uwekaji wa Daraja la Chuma kwenye MTO SUGUTI utaboresha utumiaji wa BARABARA  ya WANYERE – KATARYO.
Barabara hii ni muhimu sana kwa UCHUMI na HUDUMA za JAMII wa Kata za Tegeruka na Suguti, na kwa Jimbo letu kwa ujumla wake.
Baada ya ujenzi wa kuta imara (Abutment walls) kukamilika, Daraja la Chuma tayari limekwa na barabara imeanza kutumika.
BAJETI YA MWAKA 2021/2022
*Bajeti ya SHILINGI BILIONI 2.85 itatumika kujenga na kukarabati barabara nyingi za Jimboni mwetu
SHUKRANI:
Wananchi wa Jimbo la Musoma Vijijini wanatoa SHUKRANI nyingi sana kwa SERIKALI yetu kwa kutoa FEDHA za kujenga na kukarabati miundombinu ya BARABARA zetu za Vijijini  – AHSANTE SANA!
Taarifa kutoka:
*Ofisi ya TARURA (W)
*Ofisi ya MBUNGE
Ofisi ya Mbunge
Jimbo la Musoma Vijijini