TARURA YAENDELEA KUFANYA KAZI NZURI MUSOMA VIJIJINI

ULIMAJI na UKARABATI wa baadhi ya BARABARA za Jimbo la Musoma Vijijini unaofanywa na TARURA (W).

MENEJA TARURA (W), Injinia Abbas Hussein amesema kwamba UKARABATI wa barabara zenye urefu wa jumla ya KILOMITA 30 umepagwa ukamilike tarehe 30.6.2021
KIONGOZI huyo amezitaja barabara hizo kuwa ni zile zinazopita kwenye VIJIJI na VITONGOJI vya:
*Bukima – Bulinga – Bwasi
*Nyegugu – Rusoli – Makojo
*Busungu – Bulinga – Bujaga
*Butata – Kastam
*Kastam – Kumsoma
GHARAMA za MRADI huu ni Tsh MILIONI 90.5 (Tsh 90.5M)
BAJETI YA MWAKA 2021/2022
Barabara nyingi za Vijijini mwetu, zikiwemo za:
*MASINONO-KINYANG’ERERE
*MKIRIRA-KWANGWA HOSPITAL
zitalimwa na kukarabatiwa kwa kutumia FEDHA zilizoongezwa kwenye BAJETI ya awali ya TARURA ya Mwaka 2021/2022.
WANAVIJIJI wa Jimbo la Musoma Vijijini wanatoa SHUKRANI NYINGI mno kwa SERIKALI yetu kwa kuhakikisha kwamba BARABARA zetu zote za VIJIJINI zinapitika Mwaka mzima.
Ofisi ya Mbunge
Jimbo la Musoma Vijijini