SEKONDARI YA KATA YAJENGA MAABARA YA KIWANGO KIZURI

MBUNGE wa JIMBO, Prof Sospeter Muhongo akikakugua MAABARA ya KEMIA na VYUMBA VIPYA 4 vya MADARASA ya Dan Mapigano Memorial Secondary School ya Kata ya Bugoji.

JIMBO la Musoma Vijijini lina KATA 21 lenye jumla ya VIJIJI 68.

IDADI YA SEKONDARI JIMBONI

*21 za Kata/Serikali
*2 Binafsi
*4 MPYA zinajengwa Kabegi, Nyasaungu, Nyegina na Seka
*7 MPYA zimepangwa kuanza kujengwa Mwaka huu (2021): Bukumi, Busamba, Bwai, Kataryo/Mayani, Kurwaki/Nyang’oma, Muhoji na Wanyere.

UJENZI WA MAABARA KWENYE SEKONDARI ZA JIMBONI

*Kila SEKONDARI iko kwenye hatua mbalimbali za ujenzi wa MAABARA 3 – Biology, Chemistry and Physics

DAN MAPIGANO MEMORIAL SECONDARY SCHOOL

SEKONDARI ilifunguliwa Mwaka jana (2020) na ina jumla ya WANAFUNZI 265 (139 Form I & 126 Form II). WALIMU wapo 6 na wote wameajiriwa na SERIKALI.

WANAOTOA MICHANGO YA UJENZI WAKE
*Wanavijiji
*Serikali
*Diwani wa Kata
*Mbunge wa Jimbo
*Wazaliwa wa baadhi ya Vijiji

UJENZI uliokwishakamilika:
*Vyumba 5 vya Madarasa
*Ofisi 2 za Walimu
*Choo chenye Matundu 8

UJENZI unaondelea:
*Vyumba 4 vya Madarasa
*Maabara 3
*Ofisi 1 ya Walimu
*Choo chenye Matundu 8
*Nyumba 1 ya Walimu

Jumamosi, 27.2.2021, MBUNGE wa JIMBO, Prof Sospeter Muhongo alikagua ujenzi unaondelea kwenye SEKONDARI hii ya KATA ya BUGOJI yenye Vijiji 3 – Bugoji, Kaburabura na Kanderema.

MAABARA ZINAZOJENGWA

SERIKALI imetoa Tsh MILIONI 50 kuchangia ujenzi wa MAABARA Shuleni hapo – TUNAISHUKURU SANA SERIKALI YETU KWA MCHANGO HUU MUHIMU SANA!

WANAVIJIJI wanachangia NGUVUKAZI kwenye ujenzi wa MAABARA hizi.

MAABARA YA KEMIA

UBORA wa MAABARA hii ni wa kiwango kizuri, na ujenzi wake utakamilika kabla ya tarehe 15 Machi 2021.

Ofisi ya Mbunge
Jimbo la Musoma Vijijini
www.musomavijijini.or.tz