ZAHANATI ZA MUSOMA VIJIJINI ZAPANULIWA KWA KUONGEZA WODI ZA MAMA & MTOTO

BOMA la Jengo la Mama & Mtoto la Zahanati ya Kisiwani Rukuba, Musoma Vijijini.

Tarehe 2.2.2021
Jimbo la Musoma Vijijini

HALMASHAURI ya Wilaya ya Musoma (Musoma DC) yenye Jimbo la Musoma Vijijini (Kata 21, Vijiji 68) lina:

*Magari ya Wagonjwa (Ambulances) 5
*Zahanati 24 za Serikali zinazotoa huduma za Afya
*Zahanati 4 za Binafsi zinazotoa huduma za Afya
*Zahanati mpya 14 zinajengwa
*Vituo vya Afya 3 vinatoa huduma za Afya
*Hospitali ya Wilaya 1 – ujenzi unakamilishwa

WANAVIJIJI wa Jimbo la Musoma Vijijini wameamua kuboresha HUDUMA za AFYA zitolewazo kwenye ZAHANATI zao kwa kujenga WODI za Mama & Mtoto.

UJENZI wa MIUNDOMBINU hii mipya unachangiwa na:

*Serikali
*Wanavijiji
*Mbunge wa Jimbo
*Madiwani
*Wazaliwa wa Musoma Vijijini
*Wadau wengine wa Maendeleo

UJENZI WA WODI ZA MAMA & MTOTO

Baadhi ya ZAHANATI zilizojengwa zamani zimeanza kuboresha HUDUMA za AFYA wanazozitoa kwa kujenga WODI za Mama & Mtoto.

KISIWA cha RUKUBA ni Kijiji cha Kata ya Etaro. Kijiji hiki kimeamua kujenga WODI ya Mama & Mtoto inayotarajiwa kukamilika kabla ya tarehe 1 Machi 2021.

Zahanati nyingine zilizoanza ujenzi wa Wodi za Mama & Mtoto ni Zahanati za Bukima na Nyegina.

JENGO la WODI ya Mama & Mtoto la Zahanati ya Kisiwani Rukuba lina VYUMBA 13. Michango ya ujenzi imetolewa na:

*WANAVIJIJI – nguvukazi
*FEDHA zinazorudishwa (20% ya Makusanyo ya ushuru) kutoka Halmashauri yetu
*MBUNGE wa JIMBO – ameanza kwa kuchangia SARUJI MIFUKO 200.

WADAU wa MAENDELEO wanaombwa kuanza kuchangia VIFAA vinavyohitajika kwenye WODI hiyo, vikiwemo, vitanda, magodoro, n.k.

Ofisi ya Mbunge
Jimbo la Musoma Vijijini
www.musomavijijini.or.tz