UTEKELEZAJI WA ILANI YA UCHAGUZI YA CCM (2015-2020) NA UJENZI WA OFISI YA CCM WILAYA YA MUSOMA VIJIJINI

Mbunge wa Jimbo la Musoma Vijijini, Mh. Prof Sospeter Muhongo akikagua ujenzi wa Ofisi ya CCM Wilaya ya Musoma Vijijini inayojengwa Kijijini Murangi.

TAARIFA ZA UTEKELEZAJI WA ILANI: Jimbo la Musoma Vijijini
VOLUME I:
(Jan 2016-Juni 2020)
Ilichapishwa tarehe 7.7.2019, Kurasa 110, Rangi, Nakala 5,000 (elfu tano), zimegawiwa bure
VOLUME II:
(Julai 2019-Juni 2020), itachapishwa tarehe 30 Juni 2020
NAKALA KWENYE TOVUTI YA JIMBO
Tovuti:
Volume I: ipo
Volume II: itawekwa
UJENZI WA OFISI YA CCM WILAYA YA MUSOMA VIJIJINI
Leo, Jumamosi, 23.5.2020, Mbunge wa Jimbo la Musoma Vijijini, Prof Sospeter Muhongo AMEKAGUA UJENZI wa Ofisi hiyo inayojengwa Kijijini Murangi.
Maendeleo ya ujenzi ni MAZURI na hadi kufikia hatua hiyo ya ujenzi, Mbunge huyo ameishachangia Tsh MILIONI 12 (Milioni kumi na mbili).
SHUKRANI nyingi zinatolewa kwa KAMATI ya UJENZI kwa usimamizi mzuri wa Mradi huu. Kamati hiyo inaongozwa na Mkuu wa Wilaya (DC) ya Musoma, Dr Vicent Naano Anney.
Vilevile, SHUKRANI nyingi zinatolewa kwa WACHANGIAJI wengine wa Mradi huu (Kamati ya Ujenzi inayo majina ya wachangiaji wote)