JUBILEE YA SHULE YA MSINGI MWIRINGO YAFANA NA WANANCHI WAAHIDI KUONGEZA KASI KWENYE UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO YAO

Burudani kutoka kwa Wanafunzi wa S/M Mwiringo katika kusherehekea Jubilee ya shule yao

WANANCHI wa Kijiji cha Mwiringo, Kata ya Busambara WAMEJIWEKEA MALENGO MAPYA YA KUONGEZA KASI YA MAENDELEO YAO:
* Wataongeza kasi ya USHIRIKIANO wao na Serikali kutekeleza Miradi ya Maendeleo kijijini mwao na kwenye Kata yao.
* Wataendelea KUBORESHA MIUNDOMBINU ya Shule ya Msingi Mwiringo. Wameanza kwa kuchanga fedha za kukamilisha ujenzi wa Vyumba 2 vya Madarasa na Ofisi ya Walimu.
* Wamechanga fedha za kukamilisha ujenzi wa Vyoo vya Wavulana kwenye SEKONDARI MPYA ya Kata yao (Busambara Secondary School). Ujenzi wa Vyoo hivyo utakamilika ifikapo tarehe 24.12.2019.