JAMII IMPACT LIMITED YAKARIBISHA USHIRIKIANO NA VIKUNDI VYA UZALISHAJI

Hafla ya Uzinduzi wa Jamii Impact Limited Nyabange Mission (KMT), Musoma.

Jumatatu, 23.09.2019
Jimbo la Musoma Vijijini
Na: Fedson Masawa
Msaidizi wa Mbunge
JAMII IMPACT LIMITED ni Taasisi isiyokuwa ya Serikali inayoshirikiana na Kanisa la Mennonite UJERUMANI kupitia Mennonitisches Hilfswerk e.V. (MH) na Kanisa la Mennonite TANZANIA (KMT), na imefungua Ofisi zake Nyabangi Mission (KMT), Musoma
VIKUNDI na VICOBA  vinavyofanya KAZI za  UZALISHAJI kama vile Kilimo, Biashara, Utoaji wa Huduma za Kijamii, vinakaribishwa na JAMII IMPACT LTD kuwasilisha MAOMBI ya MIKOPO kwenye Ofisi zake.
Mkurugenzi Mtendaji wa Jamii Impact Ltd, Ndugu Mesika Mongitta, ameeleza  kwamba, “Taasisi hiyo iko tayari kufanya kazi na VIKUNDI ambavyo vinafanya MIRADI ya UZALISHAJI na vile ambavyo vinasaidia kutoa Huduma mbalimbali kwa Jamii.
MASHARTI: Waombaji wawe WANATAMBULIKA na wawe WAMEJIANDIKISHA  kwenye HALMASHAURI zao.
Ndugu Mesika Mongitta aliongezea kuwa, tayari Jamii Impact Limited imefungua Ofisi zake katika Viwanja vya Kanisa la Mennonite vilivyopo Nyabange Mission (KMT), Musoma. Hivyo, kwa maelekezo zaidi juu ya upatikanaji wa MIKOPO kutoka kwenye Taasisi hiyo.
WAOMBAJI kutoka nchini kote wanakaribishwa kuwasiliana na:
William Marcus Mdemu
Simu: 0658218673 / 0758208673
Mch John Wambura, ambae pia ni Katibu Mkuu Kanisa la Mennonite Tanzania (KMT),  anawahimiza Wana – Vikundi kutumia fursa zinazopatikana kwenye maeneo yao ili kuanzisha MIRADI inayoweza kupata MIKOPO kutoka Jamii Impact Ltd.
Hafla ya uzinduzi wa Ofisi ya Jamii Impact Ltd ilifanyika tarehe 06.09.2019 Nyabange Mission. Jimbo la Musoma Vijijini liliwakilishwa na Msaidizi wa Mbunge,  Ndugu Fedson Masawa na Wajumbe 2 (Wana-Vikundi) –  mmoja kutoka Kata ya Bugoji na mwingine kutoka Kata ya Nyakatende