SHIRIKA LA BMZ LAENDELEA KUWAWEZESHA WATU WENYE ULEMAVU NA WANAFUNZI WA JIMBO LA MUSOMA VIJIJINI

WATU wenye ULEMAVU na WANAFUNZI wakipokea VIFAA mbalimbali kutoka kwenye MIRADI ya BMZ yenye Ofisi yake pale HOSPITAL ya SHIRATI (DDH Shirati), Wilaya ya Rorya, Mkoa wa Mara

Jumanne 04.06. 2019
Na: Hamisa Gamba
Msaidizi wa Mbunge
MIRADI ya Shirika la UJERUMANI la BMZ yaendelea kutekelezwa kwenye  Jimbo la Musoma Vijijini. MIRADI hii inawalenga WANAFUNZI na WATU wenye ULEMAVU kwenye KATA 10 za Jimboni ambazo ni: Bugwema, Bukima, Bukumi, Bwasi, Kiriba, Makojo, Murangi, Nyambono, Nyamrandirira na Suguti – tukifanya vizuri BMZ huenda itapanua MIRADI yake itekelezwe kwenye Kata nyingine za Jimbo letu!
BMZ kirefu chake ni: Bundesministerium Fűr Wirtschaftliche Zusammenarbeit (German Federal Ministry for Economic Development and Cooperation).
Kati ya tarehe 28 Mei na 30 Mei 2019, MIRADI ya BMZ imekabidhi VIFAA mbalimbali kwa WATU wenye ULEMAVU na WANAFUNZI Jimboni mwetu.
Meneja wa Mradi wa BMZ, Ndugu Niwaely Sand, amekabidhi jumla ya:
(1) Mabegi ya Shule 50
(2) Daftari 100
(3) Kalamu 500
(4) Penseli 500
(5) Fimbo 10 kwa wenye ulemavu wa macho
(6) Cherehani 2
(7) Wheelchairs/Tricycles 12
(8) Miwani jozi 6
(9) Miguu Bandia 10
(10) Hearing Devices 6
Vifaa vilivyotajwa hapo juu vilikabidhiwa kwa WANAFUNZI na WATU wenye ULEMAVU ambao mahitaji yao ni MAALUM na ambao walishakamilisha VIPIMO vya kupatiwa mahitaji hayo.
Aidha Meneja huyo amewataka WATUMIAJI wa vifaa hivyo kuwa makini na waangalifu wakati watakapokuwa wanavitumia ili vidumu kwa manufaa yao.
Jimbo la Musoma Vijijini linatoa SHUKRANI za kipekee kwa BMZ na MIRADI yake yenye manufaa makubwa Jimboni mwetu – Vielen herzlichen Dank!
Let us take all plausible opportunities at Full Throttle!