UJENZI WA KITUO CHA AFYA MUGANGO: SERIKALI NA WANANCHI WAENDELEA KUSHIRIKIANA KWENYE UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO

Moja kati ya Majengo ya kituo cha afya cha Mugango

15.05.2019
Jimbo la Musoma Vijijini
Wananchi wa Kata ya Mugango WANAENDELEA kutoa SHUKRANI za DHATI kwa SERIKALI yao kwa kuwapatia Tsh Milioni 400 kwa ajili ya kupanua ZAHANATI yao na kuwa KITUO CHA AFYA chenye MAJENGO MAPYA yafuatayo:
(i) Jengo la Upasuaji (Theatre)
(ii) Jengo la Maabara
(iii) Jengo la Wadi ya Mama na Mtoto
(iv) Jengo la Maiti (Mortuary)
(v) Nyumba ya kuishi Daktari
MASHIMO 8 ya MAJI MACHAFU nayo yamejengwa.
Diwani wa Kata ya Mugango, Mhe Charles Magoma (CCM) na Mhe Kadogo Kapi, Diwani Viti Maalum (CCM) wamefanikiwa KUWASHAWISHI Wananchi Wakazi wa Kata ya Mugango KUJITOLEA kusomba MAWE (tripu 60) na MCHANGA (tripu 234) kwa ajili ya ujenzi huu ambao makadirio hadi sasa ya MICHANGO ya Wananchi na Viongozi wao (Madiwani 2 na wengine) wa Kata hiyo ni zaidi ya Tsh Milioni 32.
Daktari Kiongozi wa ZAHANATI ya Mugango, Dr. med. Marwa Saliro Mwita alieleza kwamba Zahanati yenyewe IMECHANGIA ujenzi huo kwa kulipia GHARAMA (Tsh Milioni 3.87) za usombaji wa MAJI na ununuzi wa MAFUTA ya Pampu ya Maji.
HALMASHAURI imechangia Tsh Milioni 8.
Mbunge wa Jimbo, Prof Muhongo alianza kushiriki kwenye upanuzi wa Zahanati hii kuwa KITUO CHA AFYA kwa kuchangia SARUJI MIFUKO 400.
Juzi Jumatatu, 13.05.2019, Mhe DC wa Wilaya Dr Vicent Naano Anney na Mkurugenzi wa Halmashauri Ndugu John Kayombo WALIKAGUA UJENZI wa Kituo hiki cha Afya na kutoa MAAGIZO kwa WAKANDARASI KUKAMILISHA na KUKABIDHI Majengo ifikapo Ijumaa, 17.05.2019.