UJENZI WA HOSPITALI YA WILAYA KIJIJINI SUGUTI WAENDELEA VIZURI

Maendeleo ya ujenzi wa HOSPITALI ya WILAYA Kijijini SUGUTI

Na: Verediana Mgoma
Msaidizi wa Mbunge
Wananchi wa Jimbo la Musoma Vijijini wanaendelea KUISHUKURU SERIKALI yao kwa kutoa Tsh Bilioni 1.5 kwa ajili ya ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ndani ya Jimbo lao.
HOSPITALI hiyo inajengwa kwenye Kitongoji cha KWIKONERO, Kijijini SUGUTI.
Misingi (foundations) ya MAJENGO NANE (8)  yapo hatua ya kumwaga jamvi na tayari kuanza ujenzi wa  majengo hayo ambayo ni:
(1) Jengo la Maabara
(2) Jengo la OPD
(3) Jengo la Mama na Mtoto
(4) Jengo la Madawa
(5) Jengo la Mionzi
(6) Jengo la Utawala
(7) Jengo la  Kufua Nguo
(8) Jengo la Kuchomea Taka
MATOFALI:
*Ufyatuaji wa matofali unaendelea vizuri hadi sasa yapo matofali 75,000 kati ya 85,990 yanayohitajika.
UCHANGIAJI WA MRADI:
*Wananchi wa Jimbo la Musoma Vijijini (Kata 21, Vijiji 68 na Vitongoji 374) WAMEKUBALI KUCHANGIA MRADI huu. Taratibu za Uchangiaji zimewekwa na Viongozi wa ngazi mbalimbali wanahamasisha UCHAGIAJI huu.
KARIBU NAWE UCHANGIE UJENZI WA HOSPITALI YA WILAYA inayojengwa ndani ya Jimbo la Musoma Vijijini.