KATA ZASHINDANA KUJENGA MIUNDOMBINU YA ELIMU NA AFYA NDANI YA JIMBO LA MUSOMA VIJIJINI

Boma la Zahanati ya Kijiji cha Kurwaki, Kata ya Mugango litakaloezekwa na kukamilika Machi 2019

Kwenye ziara za Ukaguzi wa Ujenzi na Uboreshaji wa Miundombinu ya Elimu na Afya, Mbunge wa Jimbo, Prof Sospeter Muhongo, ameshuhudia USHINDANI MKUBWA kati ya KATA 21 za Jimbo la Musoma Vijijini.
Leo Jumatatu, 24.12.2018 Mbunge alitembelea Kata 2 za Mugango na Nyegina na Vijiji vyake vyote.
(1) KATA YA MUGANGO
(a) Kijiji cha Kurwaki kimekamilisha Ujenzi wa Boma la Zahanati ya Kijiji chao.
Wananchi wa Kijiji cha Kurwaki WAMEDHAMIRIWA kukamilisha Uezekaji wa Jengo la Zahanati yao ifikapo tarehe 30 Machi 2019. Wanaendelea kuchangia ujenzi wa Zahanati yao. Kwenye Harambee ya leo (24.12.2018) WANANCHI wamechangia mbao, misumari na vifaa vingine vya kuezekea Jengo lao. Diwani wao, Mhe Charles Magoma amechangia BANDO 5 za MABATI. Mbunge wao, Prof Sospeter Muhongo amechangia BANDO 12 za MABATI. Kijiji cha Kurwaki kinajenga kwa kasi kubwa Zahanati yao.
(2) KATA YA NYEGINA
(a) Kijiji cha Mkiririra kilichoanza ujenzi wa Zahanati yake wakati mmoja na Kijiji cha Kurwaki, KINAENDA KWA KASI NDOGO kwa sababu ya matatizo ya Uongozi wa Mradi wa Ujenzi wa Zahanati yao. Imeamuliwa kwamba tarehe 28.12.2018 KIKAO CHA WANAKIJIJI kitakaa kutatua matatizo ya Uongozi wa Mradi wao wa Zahanati. Mbunge Prof Muhongo alishachangia SARUJI MIFUKO 200 kwenye Ujenzi wa Zahanati ya Kijiji cha Mkirira. WAZALIWA wa Kijiji cha Mkiririra na WADAU wengine alishachangia kokoto na saruji kwenye Mradi huu.
(b) Kijiji cha  Kurukerege, Kata ya Nyegina kimeamua  kuanza kujenga Zahanati ya Kijiji chao na kuikamilisha ifikapo Juni 2019.
Wananchi wameanza kukusanya vifaa vya ujenzi na watakapoanza Ujenzi wa Msingi wa Boma la Zahanati watamkaribisha Mbunge wao, Prof Muhongo, kupiga HARAMBEE YA UJENZI wa Zahanati ya Kijiji chao cha Kurukerege.