PROF MUHONGO AOMBA JINA LAKE LIACHWE NA BADALA YAKE LICHUKULIWE JINA LA MAREHEMU JAJI DAN MAPIGANO

HARAMBEE (akiwemo mbuzi) ya ujenzi wa Sekondari ya Kata ya Bugoji itakayopewa jina la Marehemu Jaji Dan Mapigano.

Jimbo la Musoma lenye Kata 21, lina Kata 3 ambazo hazina Shule za Sekondari, ikiwemo Kata ya Bugoji. Nyingine zisizokuwa na Shule za Sekondari ni Kata za Ifulifu na Busambara.
Kata za Busambara na Bugoji zimeanza kujenga kwa kasi kubwa Sekondari zao za Kata ambazo zitafunguliwa mwakani (2019).
Leo, Jumamosi, tarehe 22.12.2018 Mbunge wa Jimbo Prof Sospeter Muhongo ameendelea na  ziara zake za KUKAGUA na KUPIGA HARAMBEE za Ujenzi na Uboreshaji wa Miundombinu ya Elimu na Afya kwenye Kata za Bugoji (Vijiji 3 – Karenderema, Kaburabura na Bugoji) na Nyambono (Vijiji 2 – Saragana na Nyambono)
Wananchi wa Kata ya Bugoji wameanza ujezi wa Sekondari ya Kata yao. Ujenzi unaenda kwa kasi kubwa sana kwa kusudio la Sekondari hiyo kufunguliwa na kuanzia kutumika ifikapo April 2019.
HARAMBEE ya ujenzi wa Sekondari ya Kata hiyo imekuwa ya mafanikio makubwa. Wakazi wa Vijiji 3 vya Kata  hiyo WAMEKUBALIANA KUCHANGA Tsh 17,500 kutoka kila KAYA. Wanajitolea kusomba mawe, kokoto, mchanga na maji.
WAZALIWA na WAKAZI wa Kata ya Bugoji WAISHIO NJE ya KATA wameanza KUCHANGA KWA KASI nzuri, MICHANGO ikianzia Saruji Mifuko 50 hadi 5, na fedha kati ya Sh 500,000 (laki 5) na 50,000 (elfu 50). Baadhi ya Wachangiaji hao ni (11) –  Ndugu G Nyamohanga, S Evarist, M Kaitira, K Zakayo, A Mfungo, C  Mwesa,  M Kaitira,  M Burenga, Songorwa na M Kassim.
Mbunge Prof Muhongo amechangia SARUJI MIFUKO 100 kwenye hatua hiyo ya ujenzi.
JINA LA SEKONDARI YA KATA YA BUGOJI
Wananchi wa Kata ya Bugoji, kupitia VIKAO VYAO vinavyotambuliwa kisheria, WALIPENDEKEZA Sekondari hiyo iitwe Jina la Mbunge wa Jimbo – Prof Muhongo Secondary School – sababu kubwa ikiwa ni mchango mkubwa wa maendeleo (Elimu, Afya, Kilimo, n.k.) ambao Mbunge Prof Muhongo anautoa ndani ya Jimbo la Musoma Vijijini.
Prof Sospeter Muhongo kwa HESHIMA na UNYENYEKEVU MKUBWA alipokea OMBI HILO na yeye AKAWASHAURI na KUWAOMBA waache jina lake na kuchukua Jina la Marehemu Jaji Dan Mapigano.
Prof Muhongo kwenye ushawishi wake aliwakumbusha kwamba Marehemu Jaji Dan Mapigani alizaliwa Kijijini Bugoji, alikuwa Msomi wa Kwanza kuwa Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania wa kutoka Jimbo la Musoma Vijijini. Vilevile aliwakumbusha utendaji kazi wake (hukumu zake) uliokuwa wa kiwango cha juu ambao bado UNAHESHIMIKA hadi leo hii.
Wananchi wa Kata ya Bugoji WAMELIKUBALI PENDEKEZO la Prof  Muhongo, kwa hiyo Sekondari ya Kata ya Bugoji itapewa jina la Marehemu Jaji Dan Mapigano. Utaratibu utafuatwa.
Mbunge wa Jimbo alitembelea na kukagua Kituo cha Afya cha Nyambono kinachojengwa kwa Mchango Mkubwa kutoka kwa WAZALIWA wa Kijiji cha Nyambono. Mbali ya Mchango wake (Mbunge) wa awali wa SARUJI MIFUKO 100, leo amechangia NONDO 18 ili ufungaji wa renta ukamilike ndani ya siku 10.
Vilevile Mbunge aliongea na kusikiliza kero za Wakazi wa Kijiji cha Saragana.
Mvua zilizokuwa zinanyeesha kwa nguvu sana na kwa muda mrefu zilimzuia Mbunge kufika kwenye Shule za Msingi Kanderema, Bugoji na Kamatondo. Atazitembelea Februari 2019