ZAHANATI NYASAUNGU

Ofisi ya Mbunge inapenda kuwataarifu kuwa, kesho tarehe 15/02/2018 saa 5:00 Asubuhi, Mbunge wa Jimbo la Musoma Vijijini Prof. Sospeter Muhongo atatembelea eneo la ujenzi wa zahanati ya Nyasaungu na kuzungumza na wananchi wa kijiji hicho kuhusu utaratibu wa kuendeleza ujenzi wa zahanati yao

Katika ziara yake hiyo, Prof. Muhongo ataambatana na Mganga Mkuu wa wilaya, Madiwani n.k.

KARIBUNI NYASAUNGU

Ofisi ya Mbunge
www.musomavijijini.or.tz