MBUNGE WA MUSOMA VIJIJINI ATEMBELEA WAATHIRIKA WA MAFURIKO

Mbunge wa jimbo la Musoma vijijini Prof. Sospeter Muhongo (kushoto) akizungumza na wananchi wa kijiji cha Bukumi (hawapo pichani) mbele ya nyumba iliyoathirika na mafuriko, anayefuata ni Munubi Bunyinyiga ambaye ni mmoja wa waathirika wa janga hilo, kulia ni Katibu tarafa Adam Maungo.

Mbunge wa Musoma vijijini Prof. Sospeter Muhongo (kushoto) akiwa na Boazi Maingu, Diwani wa kata ya Rusoli (wapili kutoka kushoto) wakati wakizungumza na wakulima ambao mashamba yao yamesombwa na maji baada ya mvua kubwa iliyonyesha katika kijiji cha Rusoli kata ya Rusoli.  

Mbunge wa Jimbo la Musoma vijijini Prof. Sospeter Muhongo (mwenye fulana nyeupe) akipiga picha ya pamoja na waathirika wa mafuriko katika kijiji cha Busekera kata ya Bukumi.

Prof. Sospeter Muhongo akimjulia hali muhanga wa mvua iliyoambatana na upepo mkali katika kijiji cha Kurukerege.

Wananchi wakionesha hali halisi ilivyokuwa wakati wa tukio la Kimbunga kilichoambatana na mvua kubwa katika kijiji cha Bukumi.