MASHINDANO YA NYAMBONO NDONDO CUP YATIMUA VUMBI

Wachezaji wa moja ya timu zinazoshiriki michuano ya Nyambono Ndondo Cup timu ya Muhoji FC wakiwa kwenye picha ya pamoja.

MASHINDANO ya mpira wa miguu yanayohusisha timu 15 kutoka vijiji vya Nyambono, Bugoji na Bugwema yameanza rasmi kwenye kijiji cha Nyambono.

Mratibu wa mashindano hayo Gerlad Mbogora ambaye ni mlezi wa Urafiki FC alisema, ameamua kuanzisha mashindano hayo yanayojulikana kama Nyambono Ndondo Cup ili kuleta hamasa kwa vijana, kujitengenezea ajira, kukuza urafiki na zaidi kuwa na timu moja imara itakayoshiriki katika michuano ya mashindano ya mpira wa mguu sehemu mbalimbali jimboni na nje ya jimbo.

Mbogora alisema, pamoja na kuendesha mashindano hayo kuna changamoto ya upungufu wa mipira, hivyo mashindano hayo yanategemea mpira mmoja tu.

Mratibu huyo alimuomba Mbunge wa Jimbo la Musoma Vijijini Prof. Sospeter Muhongo na wadau wengine wamuunge mkono kwa kuwasaidia mipira miwili kwa ajili ya mashindano hayo.