JIMBO LA MUSOMA VIJIJINI – KILIMO CHA MTAMA NA MUHOGO

Mvua zinanyesha na wanavijiji wameomba mbegu za mazao ya chakula. Mbunge amekubali kuchangia upatikanaji wa mbegu hizo: (1) Mbegu za Mihogo za Sh Milioni 7 (saba) kutoka Magereza Kiabakari (Awamu I) na (2) Magunia 10 ya mtama (mbegu) ya Sh Milioni 1.2. Halmashauri itachangia usafiri na mengineyo.
Ofisi ya Mbunge