MVUA KUBWA NA UPEPO MKALI VYALETA MAAFA KWA WATU 685 KIJIJINI LYASEMBE

Ijumaa, 5.4.2024 mvua kubwa iliyoambatana na upepo mkali vilileta maafa makubwa Kijijini Lyasembe, Kata ya Murangi.

Jumla ya watu walioathirika ni: 685
Watoto 384
Watu wazima 301

Jumla ya majengo yaliyoharibika:
(i) Nyumba zilizobomoka (17):
17 za wanakijiji
(ii) Nyumba zilizoezuliwa mapaa (61):
59 za wanakijiji
2 vyumba vya madarasa ya S/M Lyasembe

Miti ya shule iliyoharibiwa na upepo mkali (40):
Miti mikubwa iliyong'olewa mizizi: 28
Miti iliyovunjiwa matawi makubwa: 12

MICHANGO KWA WAATHIRIKA
(i) Serikali ya Kijiji inaomba misaada ya aina mbalimbali hususani vifaa vya ujenzi (saruji, mabati, mbao na misumari)

Fedha za michango zipelekwe kwenye Akaunti ya Kijiji ambayo ni:
Benki: NBM
Akaunti Na: 30302300012
Jina: Kijiji cha Lyasembe

(ii) Shule ya Msingi Lyasembe
Shule hii iliyofunguliwa Mwaka 1975, kwa sasa ina jumla ya wanafunzi 811, na walimu 10.

Shule hii ina jumla ya vyumba vya madarasa 10, kati ya hayo matano (5) ni chakavu. Mawili kati ya hayo chakavu yameezuliwa mapaa! Mahitaji halisi ya shule hii ni vyumba vya madarasa 21, na nyumba za walimu 10 (two in one)

Bodi ya shule imeamua kuhamasisha wanakijiji wajenge madarasa mapya wakianza na jengo lenye vyumba viwili vya madarasa na ofisi moja.

Fedha za michango zipelekwe kwenye Akaunti ya Shule ambayo ni:
Benki: NMB
Akaunti Na: 3033700134
Jina: Shule ya Msingi Lyasembe

Wazaliwa wa Kata ya Murangi:
Wanavijiji wa Kata ya Murangi (Kata ina vijiji viwili - Lyasembe na Murangi) wanaomba Wana-Murangi wajitokeze kuchangia waathirika wa maafa yaliyoelezwa hapo juu.

Wadau wengine wa maendeleo ya Jimbo la Musoma Vijijini wanaombwa kuchangia waathirika wa maafa yaliyoelezwa hapo juu.

Picha za hapa zinaonesha:
Mkuu wa Wilaya ya Musoma (DC), Dkt Khalfany Haule (na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya), na wananchi waathirika wakiwa kwenye eneo la maafa Kijijini Lyasembe. Hiyo ilikuwa siku ya Jumamosi, 6.4.2024

Mbunge wa Jimbo la Musoma Vijijini, Prof Sospeter Muhongo akiwa shuleni Lyasembe kushuhudia uharibifu mkubwa uliobabishwa na mvua kubwa na upepo mkali. Hiyo ilikuwa leo, Jumatatu, 8.4.2024

Ofisi ya Mbunge
Jimbo la Musoma Vijijini
www.musomavijijini.or.tz

P. O. Box 6
Musoma

Tarehe:
Jumatatu, 8.4.2024